Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Ijumaa, 21 Agosti 2015

MKUTANO MKUU WA BARAZA WA BARAZA KUU LA SKAUTI TANZANIA.



Rais Kikwete (Mlezi wa Chama cha Skauti Nchini) afungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Skauti Karimjee jijini Dar es Salaam.


Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la Chama cha Skauti Tanzania umefanyika  jijini D’salaam kuanzia tarehe 13 Agosti hadi 15 Agosti 2015 katika ukumbi wa Karimjee. 

Mkutano wa Baraza Kuu hufanyika kila baada ya miaka 2 na mara ya mwisho ulifanyika mwaka 2013 jijini D’salaam, hadi kufanyika tena mwaka huu 2015 D'salaam. 

Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu ulitanguliwa na Semina Elekezi kwa wajumbe wote wa Baraza Kuu, ambao uliaanza tarehe 13 na 14 Agosti 2015 na kufuatiwa na Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu Taifa uliofanyika tarehe 15 Agosti 2015. Wajumbe wa Baraza walianza kuripoti jijini D’salaam tarehe 12 Agosti 2015 jioni. 

Wajumbe wa Baraza Kuu ni pamoja na Makamishna wote wa Skauti wa Mikoa na Wilaya za Tanzania, Wakufunzi, Viongozi wa Juu wa Chama, pamoja na wageni wengine waalikwa. 

Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu ulifunguliwa na Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete. 

Viongozi wengine wa juu wa Chama ni pamoja na Wadhamini ambao ni Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi, Waziri Mkuu Mstaafu Salim Ahmed Salim na Baba Askofu Timanywa. Rais wa Baraza la Chama cha Skauti Tanzania ni Waziri wa Elimu Mheshimiwa Dk. Shukuru Kawambwa na Makamu wake ni Kaimu Mufti wa Tanzania Alhaji Zuberi, Muadhama Kadinali Polycap Pengo na Profesa Philemoni Sarungi. 

Viongozi wengine wa Juu wa Chama ni pamoja na Skauti Mkuu wa Tanzania Mheshimiwa Mwantumu Mahiza, ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Kamishna Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mheshimiwa Abdulkarim Shah ambaye pia ni Mbunge wa Mafia na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya Taifa Mheshimiwa Balozi Mstaafu Nicholas Kuhanga. 

Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu pamoja na mambo mengine ulijadili na kupitisha Katiba ya Chama cha Skauti Tanzania, pamoja na kuchagua wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Taifa.


 

Picha zote na Murtadhwa El Bahsan

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, akiingia kwenye ukumbi wa Karimjee, wakati alipokwenda kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, akiingia kwenye ukumbi wa Karimjee, wakati alipokwenda kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Vijana wa Skauti,pamoja na skauta wakiwa wamesimama kumpokea Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, alipokuwa akiingia kwenye ukumbi wa Karimjee, kwa ajili ya kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, 
Dar es Salaam.

Skauta wakiwa wamesimama kumpokea Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, alipokuwa akiingia kwenye ukumbi wa Karimjee, kwa ajili ya kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete (wa pili kulia), akiwa na viongozi wakuu wa chama hicho, Rais wa chama, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (wa pili kushoto) na Kamishna Mkuu, Mbunge, Abdulkarim Shah (kulia) na Waziri Mkuu mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim (wakwanza kushoto) wakiimba wimbo wa Taifa, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Vijana wa Skauti,pamoja na skauta wakitoa ahadi mbele ya Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, wakati alipofika kwenye ukumbi wa Karimjee, kwa ajili ya kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Skauta, wakitoa ahadi mbele ya Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, wakati alipofika kwenye ukumbi wa Karimjee, kwa ajili ya kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Vijana wa Skauti,pamoja na Skauta wakitoa ahadi mbele ya Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, wakati alipofika kwenye ukumbi wa Karimjee, kwa ajili ya kuufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam jana.

Kamishna Mkuu, Mbunge, Abdulkarim Shah, akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.
Kamishna mkuu Mh. Abdulkarim Shah (Mb) alieleza changamoto kubwa zinazo kikakili Chama ikiwa ni pamoja na na Rasilimali Fedha pia changamoto kubwa zaidi ni kutumia nguvu kubwa na muda mwingi kutaka kuziweka mali za Chama ikiwa pamoja na kutaka kuurudisha uwanja wa Makao makuu ya Chama kwa asilimia mia moja 100% uliopo Upanga katika miliki ya Chama cha Skauti Tanzania baada ya huko nyuma kufanyika mikataba ya ubia ambayo haikua na tija kwaajili ya Chama.
Vijana wa Skauti, pamoja na Skauta wakisikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Vijana wa Skauti,pamoja na kamati ya Utendaji (Makao Makuu) wakisikiliza hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akiteta jambo na Kamishna Mkuu, Abdulkarim Shah wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Rais wa Chama cha Skauti Tanzania, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, akizungumza, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho,kabla ya kumkaribisha Mlezi wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete kuufungua rasmi Dar es Salaam.

Rais wa Chama cha Skauti Tanzania, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, akizungumza, wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho,kabla ya kumkaribisha Mlezi wa chama hicho, Rais Jakaya Kikwete kuufungua rasmi Dar es Salaam.
Nae Dk. Shukuru Kawambwa, Raisi wa Chama cha Skauti Nchini akizungumza na wajumbe wa Mkutano huo wakati wa ufunguzi aliwaambia kuwa chama kina malengo makubwa mawili, kwanza kuwaendeleza watoto na vijana kupitia mfumo wa Elimu usio rasmi ili waweze kuwa na makuzi bora kiakili, kimwili na kimaadili. Pili kuwaandaa watoto na vijana kuwa wazelendo na nchi yao, hivyo dhimaa hili kubwa na muhimu kwa mustakbali wa Taifa letu.
Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akizungumza wakati alipokuwa akiufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, akizungumza wakati akiufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete, akizungumza wakati alipokuwa akiufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.
 Aidha Rais Jakaya aliagiza kukitumia chama cha maskauti nchini kuwaanda viongozi watakao kua na hofu ya kuchukia rushwa, ufisadi na tamaa ya haraka kwa kuzingatia misngi ya maadili ya dhati kwa Taifa katika kuwahudumia wananchi, kwakua Skauti huwalea vijana katika misingi ya uadilifu hivyo ni vyema mipango hiyo ikawa endelevu haswa katika kipindi hiki cha kizazi cha leo kulingana na kasi ya kuporomoka kwa maadili. Raisi Kikwete aliyasema hayo wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania.
Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akizungumza wakati akiufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Mlezi wa Chama cha Skauti Tanzania, Rais Jakaya Kikwete (kushoto), akizungumza wakati alipokuwa akiufungua Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Waziri Mkuu mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam.

Waziri Mkuu mstaafu, Dk. Salim Ahmed Salim, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Baraza Kuu la chama hicho, Dar es Salaam jana.
Nae Waziri Mkuu mstaafu na Mdhamini wa Chama cha Skauti Tanzania aliwasihi vijana wote nchini haswa wanachama wa Skauti kuyazingatia yale aliyo yasema Rais Kikwete, pia aliiambia jamii ya watanzania watambue kua skauti inawahusu Vijana wote  wa Tanzania na haina ubaguzi wala haihusiani na masuala ya siasa.





This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 688 090 423
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania