Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Alhamisi, 8 Desemba 2016

SKAUTI WAPATA MAFUNZO YA MAWASILIANO, TEKNOLOJIA NA HABARI.














Na Rehema Ramadhani


Dar es salaam; Chama cha Skauti Tanzania kwa kushirikiana na chama cha Skauti Poland kimepata mafunzo maalum ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari maarufu kama PR-Lab  kwa baadhi ya wanachama, mafunzo hayo yalichukua takribani siku sita yalianza 27/11 hadi 2/12/2016 katika viwanja vya Jakaya Mrisho Kikwete Youth Park kilichopo Mnazi Mmoja jiji Dar es salaam.

Akizungumza na wanachama wa Chama cha Skauti Tanzania, Mratibu wa  mafunzo hayo Bi.Victoria  Drodz  kutoka Chama cha Skauti cha Poland, amesema wanafarijika kutoa elimu hiyo kwa maskauti wa Tanzania kwani Skauti ni ndugu na tunapaswa kupeana  yaliyo mazuri ili kujenga Skauti kwa pamoja.
“sisi Skauti kutoka Poland tunajiskia vizuri kuungana na kutoa elimu hii ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari.  kwa Skauti wenzetu wa Tanzania kwani Skauti hubadilishana mafunzo na ujuzi wa aina mbalimbali  kwa ajili ya kuijenga dunia zaidi ya tulivyoikuta” Alisema Bi.Victoria. 

Tumezungumza na baadhi ya wanachama wa Chama cha Skauti  Tanzania walio hudhuria mafunzo hayo na jinsi  walivyo yapokea.
‘Tumefurahi sana kwa elimu tulioipata kutoka kwa Skauti wenzetu wa  Poland kwani elimu hii hutolewa Vyuo Vikuu au kwa kulipia ili kupata elimu hii, lakini skauti wenzetu  kutoka Poland wametupa elimu hii bure  kwa ajili ya kuijenga Skauti na Dunia kwa ujumla” Alisema mmoja wa wanachama wa Chama cha Skauti Tanzania.
Tuli zungumza na Mgeni Rasmi aliyekuja kufunga mafunzo hayo Balozi Mstaafu Nicholas Kuhanga ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Utendani ya Chama cha Skauti Tanzania alisema, amefarijika  kuona vijana wake wakipewa elimu yenye viwango vya juu na anaamini kupitia vijana hao wachache waliopata elimu hiyo wataisambaza zaidi kwa Skauti wenzao na kwa vijana wote kwa ujumla. 

“Tunafarijika kuona Skauti ya Tanzania inazidi kusonga mbele na vijana wanazidi kupata elimu, hivyo kupitia vijana hawa  wachache waliopata mafunzo haya tuna imani  vijana wengine wataweza kupata  elimu hii pia tuna wakaribisha  skauti wote na kwa wale wasio kuwa Skauti katika maadhimisho ya  miaka 100 ya uskauti Tanzania ifikapo tarehe 28  Juni 2017 mkoani Arusha” Alisema  Balozi kuhanga


Balozi Mstaafu na Mwenyekiti wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Skauti Tanzania ndugu Nicholas Kuhanga akizungumza kabla ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu wa Mafunzo ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa Chama cha Skauti cha Poland na Tanzania. Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Kituo cha Michezo cha Jakaya Kikwete kilichopo Mnazi Mmoja D’salaam. 

Picha Na Mutadhwa Elbahsan






























This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 778 246 889
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania
 

Ijumaa, 2 Desemba 2016

SKAUTI WAFANYA ZIARA IPP MEDIA


Skauti wakiwa katika chumba cha habari cha magazeti ya The Guardian



Na Rehema Ramadhani
Dar es salaam; Chama cha Skauti Tanzania kiliambatana na Skauti kutoka Poland, Kenya na Burundi ambao ni washirki wa mafunzo maalum ya Public Relation, mapema jana 1/12/2016  walifanya ziara na kujione kazi mbalimbali zinazofanywa na kampuni ya IPP Media iliyopo Mikocheni Jijini Dar es Salaam.


Akizungumza na wanachama wa Skauti Tanzania, Msemaji wa  Chumba cha Habari Magazeti ya The Guardian na Nipashe  Bw. Faustin Felisian amesema wamefarijika na ujio huo wa wanachama kutoka Skauti kwa kuja kujifunza na kuona jinsi gani habari zinavyoandaliwa mpaka gazeti linapotoka mitaani.
“Tumefarijika sana kwaujio wenu katika chumba chetu cha Habari kwani ni jambo jema kujifunza na natumai wapo amabo watavutiwa na vinavyofanyika na wengine watatamani kuwa wana habari hapo baadae” alisema Bw. Felisian

Mmoja wa wanachama wa Chama cha Skauti Tanzania Ndg. Murtadhwa Rashid amesema kuwa ziara hiyo katika chombo cha habari imekuwa ya mafanikio na faida kwao kwani wamepata fursa ya kujionea mambo mbalimblai yahusuyo uandishi wa habari.
“Tumefurahi kwa kupata elimu na tumepokelewa vizuri  IPP Media. Tuna mipango ya kuifikisha Skauti yetu mbali kwa malengo ya vijana wa Taifa letu na tunawakaribisha watu wote waje kwenye uskauti tujifunze kwa pamoja” Alisema Ndg. Murtadhwa Rashid .

Picha na Nelson Opany na Ausi Hussein






This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 778 246 889
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania
 

Jumanne, 29 Novemba 2016

PUBLIC RELATION CAPACITY BUILDING WORKSHP

The Tanzania Scouts Association (TSA) in partnership with the Polish Scouting and Guiding Association (ZHP) we conducting a Public Relations capacity building workshop for 20 key staff and volunteers, youth and adults with basic and professional skills in Dar es Salaam, Tanzania. The workshop is part of the ongoing partnership activities between the two National Scout Organizations (NSOs).


The week-long workshop dubbed “PR Lab” is a training that aims to improve participant’s ability to communicate effectively and efficiently with the general public while furthering the organizations goals. It involves developing knowledge and skills in areas such as brand building, marketing theory, event promotion, social media, strategic communication, graphic design, photography, video making Blog and web design.


By the end of this workshop the participants will be able to acquire knowledge of basic marketing skills in order to properly market various Scout events; develop skills to effectively and efficiently tell Scout stories through various forms of media and media tools; as well as learn about different aspects of brand development and management. The training is being facilitated by trainers from ZHP and TSA with the assistance of the Communications & Public Relations Officer from the World Scout Bureau Africa Support Centre.


The training comes at a time when the Tanzania Scouts Association we are preparing to host different national, zonal and regional activities. From 11 to 16 December, the Tanzania Scouts Association we will host the East Africa Zonal Scout Conference, Youth Forum and Inter Patrol Scout Competitions in Arusha. On 2017 will see the Tanzania Scouts Association host the annual Africa Scout Day celebrations from 8 - 12 March in Arusha. A series of other activities have been lined up for TSA’s celebration of 100 years of Scouting in Tanzania.


PR Lab provides an opportunity for TSA to relook at our own Scout brand, develop appropriate communication and marketing strategies in order to reach out to more young people and other stakeholders through various mediums of communication. It will also be instrumental in helping the NSO to organise the different upcoming events and well as other future Scout events.
The participants will after the training form a much needed communication team that will help plan and implement TSA’s communication activities.


Photo Credits: Marek Misiurewicz (Poland Scouting & Guide Association)









This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 778 246 889
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania