Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Alhamisi, 23 Novemba 2017

Waliombeza Dk. Shika ( Bilionea wa Nyumba za Lugumi) kuumbuka, adai mabilioni yake kutua Tanzania Hivi Karibuni

Bilionea wa nyumba za Lugumi aliyeteka vichwa vya habari siku za hivi karibuni, Dk. Louis Shika, amekamilisha malipo ya bima kwa ajili ya kutumiwa fedha zake kutoka nchini Urusi..

Dk. Shika aliingia matatani baada ya kushinda mnada wa uuzwaji wa nyumba za Said Lugumi hali iliyosababisha kukamatwa na polisi, lakini binafsi alisisitiza kuwa fedha hizo anazo na sasa anaelekea kuthibitisha hilo kwa kufanya mchakato wa kutumiwa fedha.

Waandishi wa habari walimkuta Dk. Shika akiwa katika huduma za mtandao wa internet katika shirika la Posta Jijini Dar es Salaam, ambao walikuwa katika ziara ya Naibu Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi, Mhandisi Atashasta Nditiye na kujikuta hata mwenyewe akimshangaa bilionea huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumaliza kutuma taarifa za miamala hiyo, Dk. Shika amesema ametuma kiasi cha dola 100 ambapo anatarajia muda si mrefu ataweza kutumiwa fedha zake na kwenda kulipia asilimia 25 ya fedha zinazotakiwa katika nyumba hizo.
Alipoulizwa kama fedha hizo zikichelewa na kukuta mchakato huo wa malipo umepita, amesema kwa kujiamini, atanunua nyingine kwani Dar es Salaam kuna nyumba nyingi zinazouzwa siyo lazima hizo za Lugumi.

Kiasi hicho cha fedha, amekilipa kwa kwa Benki ya Equity kwenda Benki ya Bankok nchini Thailand, mchakato utakaomwezesha kutumiwa fedha zake na kuweza kununua nyumba hizo.

Katika hatua nyingine Dk. Shika alisifia huduma za shirika hilo na kueleza kwamba ndiyo hutuma huduma za internet katika kutuma nyaraka zake mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Zimbabwe: Robert Mugabe Kujiuzulu Rasmi


Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amekubali kujiuzulu kwa masharti kwamba yeye na mkewe Grace Mugabe wapatiwe kinga ya kudumu na mali zake binafsi zisiharibiwe wakati wa maisha yake yote baada ya kujiuzulu. Masharti haya yamekubaliwa na Jeshi la nchi hiyo.

Ili kubariki mchakato wa kujiuzulu ni lazima barua rasmi ya uamuzi huo ifikishwe katika ofisi ya Spika wa Bunge la Zimbabwe.




Jumamosi, 18 Novemba 2017

MAKONDA: HUDUMA A AFYA NI BURE



Madaktari Bingwa na Wataalamu wa Afya 381 kutoka Jeshi la China wanatarajia kuwasili kwa meli katika bandari ya Dar es Salaam tarehe 19 Novemba 2017 kwaajili ya kufanya matibabu bure kwa siku 7 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Mkuu a Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda katika kuhudumia wananchi.
Shime tujitokeze kwa wing ili tupate matibabu.




IJUE RSA NA HISTORIA YAKE

HISTORIA KWA UFUPI
Hapo zamani za kale palitokea kuwapo na kundi moja la wananchi. Kundi hilo lilijiunga pamoja kwenye mtandao wa Whatsapp. Malengo mojawapo ya kundi hilo ni kupashana habari za barabarani kwa minajili ya kupita mustarehe barabarani bila vizuizi vyovyote. Lakini uwepo wa kundi hilo pia ulileta fursa ya watumiaji barabara kulalamikia mambo mbalimbali yanayokera barabarani, ikiwamo mashimo, taa zisizofanya kazi, foleni, maonezi ya askari, nk. Kwa kiasi kikubwa hakukuwa na vitu vingi vya kujielimisha au kuelimishana zaidi ya kupashana habari na kushusha lawama na kutaka mambo yarekebishwe.

Mojawapo ya habari zilizo-trend sana kwenye group hilo ni kupashana habari, wapi wapo askari na wanafanya nini? Na hivyo kusaidia madereva kuwakwepa. Wanachama wa kundi walijuzana tochi zilipo, walijuzana mbinu za kukwepa foleni, mbinu za kunegotiate na askari, na hata kuwasema sana tu. Kwa upande mmoja ilisaidia sana waliomo kwenye kundi husika wasikamatwe kiurahisi.
Kwa ufupi ilikuwa kama laws of the jungle ambapo wanyama huishi kwa kuviziana.

Hata hivyo, baadae alikaribishwa katika kundi hilo kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Tanzania. Kuingia tu akashambuliwa kama mpira wa kona lakini akavumilia na taratibu akaanza kushawishi mabadiliko. Ilikuwa kazi kubadilisha mitazamo ya watu na kuwageuza kutoka walalamikaji na wakwepa mkono wa sheria kuwa waelimishaji na sehemu ya suluhisho. Yeye mwenyewe alifika wakati akachoka akakiri kwamba lile ni kundi la watu wanaolalamika tu.

Hatimaye siku ikafika, kundi hilo lililoitwa KULIKONI BARABARANI likageuka kuwa Road Safety Ambassadors na hatimaye group kubadilishwa na kuitwa RSA KULIKONI BARABARANI. Na hii ni baada ya kuungana na kundi la Facebook la Nenda kwa Usalama Barabarani December 28,2014.

KUHUSU RSA TANZANIA
RSA Tanzania ilianzishwa rasmi tarehe 28.12.2014 baada ya kufanyika mkutano mkubwa wa wanagroup la NENDA KWA USALAMA BARABARANI lililokuwepo facebook tangu 17.12.2013 mwanzilishi wake akiwa Augustus Fungo. Katika mkutano huo wa december 28.2014 mojawapo ya waalikwa walikuwa ni wanakundi la whatsapp liitwalo KULIKONI BARABARANI likiongozwa na bwana Jackson Kalikumtima. Makundi yote haya mawili yaani KULIKONI BARABARANI NA NENDA KWA USALAMA BARABARANI yaliazimia kuunngana na kuunda mtandao wa wana usalama barabarani unaoitwa RSA TANZANIA.

Kabla ya kukutana hiyo December 28, kamati ndogo ya watu wanne ikiongozwa na Augustus Fungo, iliundwa na kwenda kuuza wazo la kuwa na mkutano kwa jehsi la polisi kitengo cha usalama barabarani. Kikao cha kwanza cha kuuza wazo kilifanyika kwa Staff Officer wa Polisi Trafiki SACP Johansen Kahatano. Baada ya yeye kukubali wazo hili, alimjulisha Kamanda Mpinga, ambaye naye aliliona ni wazo zuri. Hivyo kwa pamoja tukakubaliana kuwa tarehe 28 tuwe na mkutano. Ni katika mkutano huu ndipo viongozi wa kwanza wa RSA walichaguliwa. Viongozi hao ni 

  1. Mwenyekiti wa RSA Bw. John Seka
  2. Katibu Bi Asina Omary na 
  3. Admin1 bwana Augustus Fungo.
Viongozi hawa walipewa dhamana ya kuhakikisha mtandao wa usalama barabarani unakua na kuwafikia watu wengi, na baadae unasajiliwa kuwa taasisi kamili inayotambuliska kisheria.
Katika mkutano huu, wajumbe walimuomba Kamanda Mpinga kuwa mlezi wa mabalozi wa usalama barabarani na Kamanda Kahatano kuwa Mlezi msaidizi. Majukumu ambayo waliyakubali.
Tangu wakati huo tunawaheshimu makamanda hawa kama walezi wetu, na pia makamanda wa polisi trafiki mikoa tumewafanya kuwa walezi katika ngazi ya mikoa, ila ni pale watakapokuwa wameridhia.


Tangu wakati huo RSA TANZANIA imekuwa na mahusiano mazuri na ya karibu sana na jeshi la polisi, kikosi cha usalama barabarani. Na mara kwa mara hufanya vikao na wakuu wa kikosi hicho katika ngazi mbalimbali.


WADHAMINI WA RSA TANZANIA
1. Augustus Fungo (IFM)
2. Jackson Kalikumtima(Private Sector)
3. Ally Nurdin (Unilever Tanzania)
4. Gibson Urassa (UNHCR)
5. Mohammed Mpinga (Police Tanzania)
6. Johansen Kahatano (SUMATRA)
7. Marlin Komba (Wizara Mambo ya Ndani)
8. John Seka (Law School of Tanzania)
9. Adam Phillip (TIB)
10. Asina Omary (Kitivo cha Sheria, UDSM)


BODI YA WAKURUGENZI - WAKURUGENZI WATENDAJI.
Yaani hawa ni wale waliopo kwenye majukumu ya kila siku ya uendeshaji.
1. Augustus Fungo-Taaluma: Sheria
2. Jackson Kalikumtima-Taaluma: Mhasibu
3. Asina Omary-Taaluma: Sheria
4. John Seka-Taaluma: Sheria
5. Ally Nurdin(Six)-Taaluma: Transport and Logistics


KANUNI ZETU ZA MIJADALA HIZI HAPA CHINI (KANUNI KUU 20 ZA RSA TANZANIA)


Katika majadiliano yoyote inayoendeshwa katika majukwaa ya RSA, yawe ya mtandaoni au ya nje ya mtandao, kila RSA atazingatia kanuni na miongozo ifuatayo:

1. HABARI SAHIHI:
Hairuhusiwi kuandika habari yoyote isiyo ya ukweli ama ya kufikirika tu na kuipa uhai kuwa ya kweli.

2. UHAKIKA WA TAARIFA:
 Thibitisha taarifa kabla hujaituma na kama huna uhakika sema “sent as received, for verification”au “Habari hii Haijathibitishwa”. Hapa utaeleweka kuwa unataka jambo lifuatiliwe kujua ukweli wake na kwamba wewe si chanzo halisi cha taarifa.

3. UKAMILIFU WA TAARIFA:
 Ripoti tukio kwa kutoa taarifa inayojitosheleza kwa kutaja nani muhusika (jina/namba ya gari/uelekeo), nini kimetokea, wapi limetokea, na ungependa nini kifanyike.

4. HABARI ZILIZOKATAZWA:
Ni marufuku kupost habari zinazohusu siasa, vichekesho, matangazo ya kibiashara, michezo, muziki, dini au habari binafsi labda kama zimetokea barabarani mf.ajali, homa, kuibiwa, breakdown, na kubambikiwa kosa/jinai. Kama huna hakika na habari tafadhali, mtumie admin inbox kwanza.

5. KUHUSU SALAMU:
 Unapoingia kundini kila siku kwa mara ya kwanza, unaruhusiwa kutao salamu na kisha kuendelea kutoa habari. Mf. Habari za asbh rsa, njia ya makongo iko shwari, au hapa Arusha kuja jama maeneo ya sekela.

6. TAARIFA ZA KIPAUMBELE:
 Taarifa tunazozipa kipaumbele hapa ni zinazohusu msongamano wa magari ili kuwasaidia TCC kujua kwa kuelekeza nguvu kazi; ajali; ukiukaji sheria barabarani; utendaji mbovu wa askari. Aidha UKIMYA wa muda mrefu bila kutoa taarifa au kucnagia mada kwa mwezi mmoja na Zaidi hatutavumilika.

7. UUNGAJI WA WANACHAMA: Huruhusiwi kumwongeza mjumbe yeyote bila ruhusa ya admin na bila kwanza kumwelezea huyo mjumbe mpya nini kinachofanyika hapa rsa. Aidha mtu anayemwombea mtu mwingine uanachama ni sharti ahakikishe anampa mtu huyo kanuni na azikubali, amweleze kuhusu wajibu wake wa kuwa active, na kuzingatia kanuni.

8. WAJIBU WA RSA:
Kuwa RSA ni kuwa mstari wa mbele katika kutii sheria za barabarani; kukiri kosa na kulipa faini au kuomba radhi; kujitolea; kutoa taarifa za barabarani; kujielimisha na kuwaelimisha wengine. RSA hayuko hapa ili kuwa juu ya sheria au kuwa uchochoro wa kuombea feva bila kuwajibika, pia usitake attention ambazo si za lazima.

9. PICHA:
Hairuhusiwi kuweka picha mbaya za ajali zisizowastahi marehemu. Picha yoyote unayoweka humu au video sharti iwe ina maelezo yanayojitosheleza kuelimisha au kuchukua hatua. Pia si ruksa kurudia rudia mara nyingi kutuma picha hizo hizo au zinazotoa ujumbe mmoja iwapo ulizotoa awali zinajitosheleza.

10. KAULI/LUGHA YA MAWASILIANO:
Lugha ya Matusi, vijembe, siasa hairuhusiwi katika foram za RSA, wala ubishi usio wa hoja. Siku zote usinungĂșnike, lalamika kwa kutoa hoja na ikiwezekana pendekeza suluhisho.

11. TRAFIKI JAMII:
RSA sio Polisi wala jasusi yeye ni trafiki jamii na ataendelea kuwa trafiki jamii kazi kubwa ni kutii sheria, kujielimisha na kuelimisha, na kutoa taarifa na kuchochoe mabadiliko. Hatuhitaji shujaa mfu (dead hero), usihatarishe maisha yako au usalama wako kwa kupiga picha au kushughulika na tatizo/suala lililo nje ya uwezo wako. Toa taarifa tu.

12. UONGOZI:
Rsa inaongozwa kwa sheria na kanuni. Ni marufuku kujiamulia mambo bila kupata Baraka za uongozi yaani Mwenyekiti, Katibu, Mlezi au Admins. Na kwa upande wa matawi ya RSA mikoani, kila tawi litazingatia mamlaka yaliyo kwenye himaya yake na kuheshimu mamlaka ya taifa.

13. RUFAA/MALALAMIKO:
 Ikiwa utaona umeonewa iwe kwa kufungiwa au kukanywa basi unaruhusiwa kulalamika kupitia mmoja wa wanachama ili alifikishe barazani watu waweze kujadili. Vivyo hivyo ukifungiwa unaweza kupitai mjumbe mmoja wapo au admins kuomba msamaha na kuandika ujumbe wa kuomba kurejeshwa kundini, na kwa masharti utakayopewa.

14. MAAMUZI YA ADMINS:
 Wakati wowote na wanapoona inafaa admins wanaweza kuchukua hatua yoyote kwa mwanachama atakayekiuka utaratibu. Hatua zinaweza kuwa onyo, karipio, au kusimamishwa kwa muda. Admins hawaruhusiwi kutofautiana hadharani isipokuwa inbox.

15. SIRI/USALITI:
 kila rsa ana wajibu wa kutunza siri za kundi zin
azohusiana na taarifa za uvunjifu wa sheria za barabarani.
 Kumtaja mtoa taarifa au kuvujisha utambulisho wake kwa mkosaji ni kosa na ni usaliti na yeyote atakayefanya hivyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.

16. VITISHO:
ni marufuku rsa yeyote kujaribu ama kumtisha mwenzake inbox au kwa sms au kwa simu au njia nyingine yeyote ila kwa sababu tu ya jambo alilolisema au taarifa aliyoitoa humu inayoenda kinyume na maslahi ya mtishaji au mtuhumiwa.

17. MARUFUKU:
Ni marufuku kwa RSA yeyoye kutumia Uanachama wake kwaajili ya kulinda maslahi yake binafsi, kutisha, kudhoofisha juhudi za RSA, kupotosha, kutotii sheria, kuomba upendeleo maalumu, kudhalilisha  au kuhujumu juhudi zozote za RSA.Kufanya hivyo ni kosa na hatua za kinidhamu zitachukuliwa mara moja.

18. UTII WA SHERIA:
Kila RSA atawajibika kikanuni na kisheria kutii sheria za barabarani kwa yeye kuwa mfano wa kuigwa na mwingine. Mathalani pale atakapopigwa faini kwa kosa halali alilolitenda, hatakiwa kubisha bali kulipa, na pale atakapokuwa amesingiziwa kosa ambalo hajalitenda au halieleweki basi ataomba ufafanuzi ngazi kwa ngazi au kutoa taarifa kwa uongozi wa RSA ilia pate kushauriwa na kusaidiwa.

19. MAHUSIANO MEMA:
Siku zote RSA wataishi, kuhusiana na kuheshimiana kama familia, watakuwa tayari kusaidiana na kushirikishana mambo mbalimbali ya kimaendeleo, ya kihuzuni na kifuraha. Endapo RSA anasafiri kwenda mkoa wowote au sehemu yoyote nchini, atajitahidi kuwaarifu na kuwatafuta RSA waliopo eneo analokwenda ili kukuza mahusiano mema na kubadilishana mawazo.

20. ADHABU:
Mtu yeyote akakayekiuka kanuni hizi, kulingana na ukubwa wa kosa, anaweza kusimamishwa jukwaani au kwenye mjadala mara moja na kupelekwa kwenye kamati ya nidhamu ambako suala lake litajadiliwa na kutolewa maamuzi. Utaratibu huu utawahusu wanachama wanaotumia mitandao ya telegram na whatsapp na mwingine wowote unaofanana na huo, kwa wale wa facebook wanaweza kuondolewa moja kwa moja baada ya kupewa onyo na kutotii. Mtu yeyote atakayesaliti harakati za RSA atashughulikiwa kinidhamu na adhabu yake inaweza kuwa kufutwa uanachama au kusimamishwa


MATUKIO MBALI MBALI KATIKA PICHA








This Blog Powerd by:
  Elbahsan Web & Blog Designer
A Subsidiary of  Elbahsan Web & Blog Designer for Global Development, Inc.
+255 (0) 653 373 432 & +255 (0) 778 246 889
For the Web & Blog Template and Designing
Dar Es Salaam, Tanzania


Jumamosi, 8 Julai 2017

SIKU YA MABALOZI WA USALAMA BARABARANI YAFANYIKA KITAIFA MKOANI DODOMA



Naibu waziri wa Ulinzi Mhandisi Hamad Masauni ambae pia ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na Usalama Taifa(Mwenye T-Shirt ya Blue) akiwa ameambatana na kamanda wa kikosi cha usalama barabarani nchini DCP Mohammed Mpinga ambae pia ni katibu wa Kamati ya usalama barabarani na Mlezi wa RSA Tanzania wakiwa wanaingia uwanja wa Mashujaa mjini Dodoma baada ya kupokea maandamano ya Mabalozai wa usalama Barabarani yaliyofanyika mapema leo Mjini Dodoma (Makao makuu ya Nchi). Picha na Murtadhwa Elbahsan / Vero Ignatus

 Na.Murtadhwa Elbahsan / Vero Ignatus 
Siku ya mabalozi wa usalama barabarani (RSA) imefanyika Kitaifa mkoani Dodoma ambapo Naibu waziri wa Ulinzi Mhandisi Hamad Masauni amekuwa mgeni  rasmi, shughuli hiyo imefanyika katika viwanja vya mashujaa na imewashirikisha mabalozi mbalimbali Tanzania bara na Visiwani.

Mwenyekiti wa mabalozi wa usalama Taifa John Seka amesea kuwa lengo kuu la siku hiyo ni kuweza kuleta uhamasishaji kwa wananchi  ili waweze kupata elimu ya usalama barabarani na wasione ni jukumu la jeshi la polisi peke yake, kukuza mahusiano na jeshi la polisi  pamoja na mabalozi kufahamiana zaidi na kuwapongeza mabalozi kwa kazi nzuri ambayo wanayoifanya ya kujitolea. 

Kwa upande wake kamanda wa Kikosi cha usalama barabarani  ambae pia ni katibu wa Baraza la usalama barabarani Taifa DCP  Mohammed Mpinga  amesema kuwa takwimuza vifo na majeruhi zinaonyesha kuwa nchi zinazoendelea zinaathirika sana na tatizo hili hivyo bado tunalo jukumu kubwa la  kupingana na ajali za barabarani
Ameainisha takwimu za ajali kuanzia mwaka 2014 hadi mwaka 2017 zimepungua kwa asilimia 44  vifo vimepungua 13% majeruhi 30% ambapo wa asilimia kubwa RSA inahusika kwa kiwango kikubwa kutoa taarifa kwa jeshi la polisi  changamoto  kutambua juhudi za usalama barabarani wanaojitole.

Mpinga ambae  pia ni mlezi wa( RSA)amewapongeza mabalozi hao kwa kazi nzuri wanayoifanya  kwa kukabiliana na ajali za barabarani kwa kuonya kukaripia pale wanapoana mwenendo mbaya wa madereva pamoja na kutoa taarifa kwa jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani
“ Muendelee kujitoa kama vile ambavyo mnavyojitoa  kwani mnalirahisishia kazi jeshi ,mmekuwa mkiokoa maisha ya watu wasife kwa uzembe kwaajali za kujitakia “alisema .

Amezitaja changamoto zinazowakabili ni pamoja na vifaa vya lkutendea kazi,ubovu wa barabara na miundombinu,ukosefu wa alama za barabarani,utashi wa kisiasa ,wadau wanaona suala la usalama barabarani siyo la kwao na haliwahusu.

Mkuu wa kitengo cha Elimu nchini Tanzania ASP Mosi Boniface Ndozero  amesema kuwa mambo mawili lazima yazingatiwe, “ni vyema kuzingatia na kufuata alama za usalama barabarani yote yakizingatiwa ajali  zitapungua kabisa” amesema kuwa jeshi lapolisi nchini kitengo cha elimu limejipanga vilivyo kuhakikisha kuwa elimu wanayoitoa  inawafikia walengwa pamoja na hayo amesema jeshi la polisi limejipanga  kutoa elimu kwa wanafunzi mashuleni kuhusu elimu ya usalama barabarani 

Kwa upande wake  Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma SACP Lazaro Mambosasa  amesema kuwa wanamipango  endelevu  katika mji wa Dodoma  ili ujio wa serikali usije ukaongeza vifo na ajali kwani wamejipanga kuthibiti ajali za barabarani   

Ikumbukwe kuwa RSA imesajiliwa rasmi mwaka 2014 kama taasisi isiyo ya kiserikali ikiwa na wanacham 10 hadi sasa wapo zaidi ya 60,000 kwenye majukwaa ya mitandao wa kijamii (Whatsap, Facebook, Twitter, Instagram nk.), wapo wakurugenzi 8, kanda 5ambazo ni kanda ya kusini, kanda ya kati, kanda ya kaskazini ,kanda ya mashariki,kanda ya ziwa na kanda ya nyanda za juu kusini, wapo maadimini 20 kwenye majukwaa hayo ya mitandao ya kijamii.














Alhamisi, 15 Juni 2017

Tundu Lissu,Abdallah Mtolea Wapinga Azimio la Bunge Kumpongeza Rais Magufuli

Azimio la Bunge la kumpongeza Rais John Magufuli kwa hatua anazochukua kukabiliana na upotevu wa mapato ya serikali katika sekta ya madini jana liligawa Bunge baada ya wabunge wa upinzani kulikataa wakati wenzao wa CCM wakilikubali.

Mwenyekiti wa Bunge, Musa Zungu alipowahoji wabunge kama wanakubali azimio hilo, wabunge wote wa CCM waliitikia "ndiyooo" wakati wale wa upinzani walisema "siyooo".

Azimio hilo lenye kurasa mbili liliwasilishwa bungeni jana na Mbunge wa Newala Mjini (CCM), George Mkuchika na baada ya hapo wabunge walipata nafasi ya kulijadili.

“Bunge linamuunga mkono Rais John Magufuli na lipo tayari kutoa ushirikiano wa dhati kadri itakavyohitajika kuhakikisha juhudi hizi hazipotei bure na sekta ya madini inachangia maendeleo ya wananchi na Taifa kwa ujumla,” alisema Mkuchika ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki, Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge.

Lakini, aliposimama akiwa wa kwanza kuchangia hoja ya maazimio hayo, Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu alipinga akisema ni kinyume na majukumu ya Bunge hivyo kulitaka lisiendelee na taratibu za kumpongeza Rais akisema alichokifanya si kipya.

“Kazi ya Bunge ni kuishauri Serikali, siyo kuipongeza au kuiimbia mapambio. Hili siyo azimio la Bunge, bali wana-CCM kumpongeza mwenyekiti wao,” alisema mnadhimu huyo wa Kambi ya Upinzani Bungeni.

Alisema kinachofanywa na Rais Magufuli kilifanywa pia na watangulizi wake waliounda tume kadhaa na kwamba mpaka azimio hilo linajadiliwa, bado usafirishaji wa dhahabu inayochimbwa kwenye migodi mbalimbali nchini unaendelea.

“Dhahabu na madini mengine yanaendelea kusafirishwa hivi sasa. Ripoti za Profesa Mruma na Profesa Osoro ni professorial rubbish. Ni uongo, uongo, uongo,” alisema Lissu.

Ingawa alitakiwa kufuta neno rubbish kwenye mchango wake, Lissu alifafanua kwamba ripoti za wenyeviti hao wa kamati mbili za Rais za kuchunguza makontena 277 ya mchanga wa dhahabu, hazina taarifa sahihi.

Kuhusu azimio hilo kutokuwa na jipya, alisema Rais mstaafu, Benjamin Mkapa aliunda kamati ya Jenerali (Robert) Mboma mwaka 2002, ya Dk (Jonas) Kipokola mwaka 2004 kisha ya Dk (Enos) Bukuku mwaka 2005. Alisema hata Rais wa Awamu ya Nne, Jakaya Kikwete naye aliunda mbili za Lawrence Masha na Jaji Mark Bomani.

Alisema kama Bunge linataka kupongeza kuhusiana na kamati zilizoundwa na Rais Magufuli, basi halina budi kuanza na watangulizi hao ambao walifanya kama anachokifanya sasa kwa masilahi ya Taifa huku akipendekeza semina itolewe kwa wabunge ili kuwaongezea uelewa wa masuala ya madini na kuwafanya wachangie wakiwa na ufahamu wa kutosha kuhusu sekta hiyo.

Lissu alipingwa na Mbunge wa Mtera (CCM), Livingstone Lusinde ambaye alitoa sababu za kumpongeza Rais Magufuli akisema kuna tofauti kati ya kamati alizoziunda na zile za watangulizi wake.

“Rais ameenda mbali zaidi. Ripoti imepokewa hadharani na wananchi wote wameisikia. Hii ni hatua ya mbele. Haiwezekani Taifa lisimpongeze Rais anapofanya mambo yanayoonekana,” alisema.

Alisema ameona clip (video fupi) za mawaziri wakuu wastaafu waliohamia upinzani; Edward Lowassa na Frederick Sumaye wakimpongeza Rais kwa hatua zake.

Lakini, Mbunge wa Temeke (CUF), Abdallah Mtolea alionekana kuungana na Lissu akiongeza kwamba maazimio hayo hayakuwa sawa kwa maelezo kwamba kilichofanywa na Rais Magufuli mpaka sasa hakijapiga hatua kubwa zaidi ya kilichofanywa na watangulizi wake.

Alisema suala la msingi ni kudhibiti wizi wa rasilimali nchini akikumbusha kwamba Kikwete pia aliunda tume lakini hata baada ya kupelekewa ripoti, hakufanya chochote hatua ambayo Rais Magufuli amefikia mpaka sasa kwenye vita aliyoianzisha.

Alisema hoja ya wizi wa madini ilianzishwa siku nyingi na wabunge ambao walionekana kuwa si wazalendo. “Kama Mkapa na Kikwete tungewapongeza kwa kuunda tume leo ingekuwaje? Bunge tusiwe washangiliaji,” alisema.

Alikumbusha pia kwamba Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba alipiga kelele, Dk Hamis Kigwangallah wa Nzega Vijijini (CCM) aliteswa, Tundu Lissu, Zitto Kabwe wa Kigoma Mjini (ACT Wazalendo) na John Mnyika wa Kibamba (Chadema) walilizungumza suala hilo lakini walibezwa.

Alisema kwa kuwa suala hilo sasa linazungumzwa na mtu anayependwa, linaungwa mkono.

Katika mchango wake, Hasunga ambaye ndiye aliyekuwa mtoa hoja alisema hatua ya Rais kuzuia usafirishaji wa mchanga nje ni muhimu inayopaswa kuungwa mkono na Watanzania wote.

“Jimboni na mkoani kwangu kuna madini mengi, hatustahili kuwa maskini,” alisema.

Akiunga mkono hoja hiyo, Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola alisema anachokifanya Rais Magufuli ndicho alichoahidi hata kabla hajashika wadhifa huo,

“Aliahidi watu watalima kwa meno, tunaona mafisadi wakilima kwa meno. Namuomba hata watu wanaowatetea wezi hawa awalimishe kwa meno pia.”

Mbunge huyo ambaye aghalabu huzungumza kwa mbwembwe aliungwa mkono na Mbunge wa Rufiji (CCM), Mohamed Mchengerwa ambaye alitaka neno uzalendo liondolewe kwenye kamusi ya Kiswahili endapo kuna mtu atapinga yanayofanywa na Rais Magufuli.

“Tunaamini mambo haya yakitekelezwa vyema tutakuwa na barabara za lami na hatutakuwa na deni la Taifa,” alisema Mchengerwa.

Serikali Yatoa Onyo.......Yavitaka vyombo vya habari kuacha kuwahusisha Marais wastaafu na mchanga wa madini

Serikali ya Tanzania kupitia Waziri ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo imevitaka vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuacha kuwatuhumu Marais wastaafu kwenye sakata la mchanga wa madini kwani majina yao hayajatajwa kwenye ripoti ambayo Rais Magufuli ameipokea.

Katika taarifa ambayo imetolewa na Waziri Mwakyembe imeeleza kuwa kuna baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii wamekuwa wakituhumu Marais wastaafu bila kujua athari zake kiasiasa na kijamii 
 

Viongozi wa Dini Watangaza Siku Saba za Kumwombea Rais Magufuli

Na Jonas Kamaleki- MAELEZO
Viongozi wa dini wametangaza maombi ya siku saba nchi nzima kumwombea Rais John Pombe Magufuli ili aendelee na juhudi zake za kulinda raslimali za watanzania kwa manufaa ya Taifa kwa ujumla.

Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam katika mahojiano maalum na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote, Askofu William Mwamalanga kwa niaba ya viongozi wa dini.

“Tumeamua kufanya maombi ya siku saba kwa kumtaka kila mtanzania popote alipo kutembea hatua saba kila siku akimwombea Mhe. Rais Magufuli ili Mungu amlinde pamoja na anaofanyanao kazi kwa usahihi (uaminifu)”, alisema Askofu Mwamalanga.

Ndani ya siku hizo saba kila mtanzania atakuwa ametembea jumla ya hatua 49 akimwombea Rais Magufuli na wazalendo wenzake.

Kwa mujibu wa Kiongozi huyo wa Dini, maombi hayo yataanza leo Alhamisi Juni 15 nchi nzima na yatajumuisha watu wa dini zote nchini, yaani madhehebu ya Kiislam, Kikristo, Kihindu, Budha na madhehebu mengine.

Maombi haya yanafanyika baada ya kuona kuwa Mhe. Rais Magufuli anachukua hatua madhubuti za kutaka waliohusika kwa namna yoyote kuiba raslimali za Taifa hususani madini, wanachukuliwa hatua na kuitaka kampuni ya ACCASIA kulipa kile ambacho walichukua kinyume cha sheria.

Askofu Mwamalanga alisema kuwa Kamati yake inamwomba Rais Magufuli achukue hatua za haraka kudhibiti raslimali za nchi kwa upande wa Wizara ya Maliasili na Utalii ambako mali nyingi zinatoroshwa na wajanja wachache.

Kamati hiyo ya Kitaifa ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa jamii ya dini zote imemwomba Mhe. Rais aziunganishe Wizara za Nishati na Madini na Maliasili na Utalii na kuunda wizara moja ambayo itasimamia kwa karibu raslimali za watanzania.

“Tunamwomba Rais Magufuli amchague mtu makini na mzalendo mwenye uchungu na nchi hii ili asimamie wizara hiyo, na nina hakika wizara hiyo ikisimamiwa vizuri, ndoto ya Rais ya kuifanya Tanzania kuwa nchi mhisani itatimia kwa kuwa hapa Mungu ametujalia kila kitu”,alisema Askofu Mwamalanga.

Viongozi hao wamempongeza Rais Magufuli kwa Uzalendo na Ujasri alionao katika kulinda raslimali za Taifa na kupambana na maovu. Wamesema ni kiongozi wa kuigwa na Marais au viongozi Duniani kote.

Kuhusu suala la walioachishwa kazi kutokana na kuwa na vyeti feki, Askofu Mwamalanga alisema kuwa Kamati inamwomba Mhe Rais kuwasamehe wale ambao wameitumikia nchi hii kati ya miaka mitano na 30 ili walau wapatiwe kifuta jasho licha ya kwamba walitumika bila kuwa na vyeti halali vya Kidato cha nne.

“Msamaha tunaoomba si wa kuwarudisha kazini bali tunaomba kwa ajili ya kupata kiinua mgongo kwani wengine walitumika kwa uaminifu na hata kupewa tuzo za ufanyakazi hodari (bora) hasa katika sekta za Afya,wauguzi, Elimu na maeneo mengine”, alisema Askofu Mwamalanga.

Mapema wiki hii, Rais Magufuli alipokea ripoti ya pili ya uchunguzi wa makinikia ambayo iliwajumuisha wanasheria na wachumi. Katika ripoti hiyo ilibainika kuwa kiasi kikubwa cha madini kilichukuliwa bila watanzania kupata chochote. Takriban madini yenye thamani ya shilingi trilioni 108 yalisafirishwa nje ya nchi bila Tanzania kupata faida kutokana na madini hayo.

UKATILI: Msichana Asimulia Jinsi Kondakta na Dereva Walivyombaka Kwa Zamu Ndani ya Daladala

Dereva na kondakta wa daladala zinazofanya safari ndani ya Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro, Soweto–Mbuyuni wanatuhumiwa kumbaka abiria wao kwa zamu na kumuumiza sehemu za siri.

Tukio hilo lililotokea Juni 12 saa moja jioni maeneo ya Veta katika uchochoro uliopo karibu na shule ya Northen Highland iliyo umbali wa mita 400 kutoka barabara ya lami.

Akielezea tukio hilo, binti huyo mwenye umri wa miaka 20 alisema alitumwa na bosi wake kwenda kununua mahitaji ya nyumbani Soko la Mbuyuni na kumuelekeza kuwa akimaliza apande basi la Soweto sokoni hapo na ashukie mwisho ambako angechukua bodaboda ya kumfikisha nyumbani.

“Nilipomuuliza konda akaniambia ndiyo na nikampigia bodaboda ambaye nilipewa namba na bosi wangu ili ampe maelekezo huyo kondakta sehemu ambayo watanishusha ili yeye anichukue hapo na wakazungumza na baadaye akanirejeshea simu yangu,” alisema msichana huyo.

Alisema baada ya hapo safari ya kutoka Mbuyuni kwenda Soweto ilianza.

“Kwa kuwa nilikuwa mgeni, sikuelewa hata kituo kipi cha kushukia. Niliendelea kukaa hadi nilipoona watu wote wameisha kwenye (Toyota) Hiace, ndipo nikamuuliza konda kwa nini hanishushi akasema bado sijafika,” alisema.

Anasema alishangaa kuona dereva anaenda kuegesha gari uchochoroni na aliposimama, kondakta akashuka, akidai anaenda kujisaidia. “Aliporudi kwanye gari alifunga mlango na wakazima taa na kuanza kuniambia kuwa wamenipenda kama ninataka kuwa hai nikubaliane na wanachokitaka na nikikataa wataniua,” alisema binti huyo.

Alisema baadaye dereva alitoka kwenye usukani na kumfuata alipokaa na kuanza kumpapasa.

Alisema alipoona hivyo alijaribu kutoka nje kupitia dirishani, lakini walimvuta ndani huku wakimfunga mdomo asipige kelele na kumtishia kumuua.

“Nilikubali yaishe na nikatulia. Akaanza dereva huku kondakta akinishika mikono na baada ya kumaliza alichofanya, konda naye akaja akafanya hivyohivyo. Nilisikia maumivu, lakini nilishindwa kupiga kelele kwa kuwa walinitisha kuwa wangeniua,” alisema dada huyo.

“Walipomaliza kufanya ukatili huo, konda alimwambia dereva kuwa waniue kwa kuwa nimeshawatambua, lakini dereva akasema hakuna haja.”

Alisema katika mabishano hayo alijikaza na kuwaambia kuwa yeye ni mgeni na hajui popote kwa hiyo hatamwambia mtu kwa kuwa hilo ni tukio la aibu.

“Walikubaliana na mimi na wakaniambia kuwa ni kweli kubakwa ni kitendo cha aibu kwa hiyo nikimwambia mtu nitatengwa na jamii. Nikawaomba wanisaidie sehemu ya kupata msaada niweze kufika nyumbani,” alisema.

Alisema baadaye aliwaomba aende kuchukua kiatu chake kilichokuwa kimedondoka dirishani wakati akitaka kuruka, na walipomruhusu akatumia nafasi hiyo kusoma namba za gari.

Mlezi wake, Abdi Massawe alisema baada ya kufika nyumbani akiwa na bodaboda, binti huyo alimweleza tukio hilo na akatoa taarifa polisi ambako alipewa fomu ya matibabu aliyoitumia Hospitali ya Mawenzi, ambako vipimo vilithibitisha kuwa alibakwa.

“Huyu binti ni mgeni kutoka mkoani Singida. Hapa Moshi ana mwezi mmoja tu,” alisema Masssawe.

Massawe alisema baada ya hapo alianza kusaka daladala hilo kwa kutumia namba alizopewa na binti huyo na kufanikiwa kuikuta maeneo ya Soweto. Baadaye aliwapigia simu polisi ambao walifika na kushusha abiria waliokuwamo na kuipeleka kituoni.

Alisema wakati dereva akiendelea na mahojiano kondakta alitoroka.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita alisema derava wa gari hilo aliyemtaja kuwa ni Salimu Abdalla (30) anashikiliwa na polisi ambao wanaendelea kumtafuta kondakta ambaye alitoroka akiwa katika kituo cha polisi.

Kwa sasa binti huyo anatibiwa Hospitali ya Mawenzi.

Jumanne, 13 Juni 2017

Prof. Muhongo, Andrew Chenge na Wahusika Wengine Wazuiwa kutoka nje ya Mipaka ya Tanzania

Serikali imeagiza, Mawaziri, Wanasheria Wakuu wa Serikali na Manaibu wao, Wakurugenzi wa idara za mikataba, na Makamishna wa madini, wanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini na watumishi wengine wa Serikali na watu wote waliohusika katika kuingia mikataba ya uchimbaji madini, utoaji wa leseni za uchimbaji wa madini na kuongeza muda wa leseni, watumishi na wamiliki wa makampuni ya madini kuto toka nje ya mipaka ya Tanzania.

Agizo hilo lilitolewa jana  na Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ambaye alisema kuwa, wote waliotajwa kuhusika katika kulisababishia taifa hasara kupitia sekta ya madini, hawaruhusiwi kutoka nje ya mipaka ya Tanzania isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini.

“Naelekeza wote waliotajwa kuhusika hakuna kutoka nje ya mipaka ya nchi yetu isipokuwa kwa kibali maalum kutoka serikalini. Vyombo vitekeleze maagizo ya Rais kwa utimamu,” aliandika Waziri Nchemba kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii.

Agizo hili limekuja ikiwa ni saa chache tangu Rais Magufuli alipoagiza kuwa, viongozi wote na watumishi mbalimbali waliohusika katika kusaini mikataba mibovu na kushiriki kwa namna yoyote ile, wahojiwe.

Miongoni mwa watakaoathiriwa na zuio hilo, ni pamoja na Maafisa wa TRA, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Andrew Chenge, Mwanyika, na Werema, Mkurugenzi Idara ya Mikataba, Mary Ndosi, Kamishna Dalali Peter Kafumu, Waziri Prof. Muhongo, Waziri Daniel Yona, Waziri Nazir Karamagi, Jaji Julius Malaba, Waziri William Ngeleja.

Awali Waziri Nchemba alimpongeza Rais Magufuli kwa jitihada alizozichukua katika kuhakikisha analinda rasilimali za wanyonge na kusema kuwa hakuna uzalendo kama huo.

“Hakuna uzalendo zaidi ya kulinda rasilimali za Taifa, Hakuna utetezi wa wanyonge zaidi ya kulinda rasilimali zao.Hongera sana Mh.Rais kwa uzalendo wa vitendo kwa Taifa letu.”