Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumatatu, 29 Mei 2017

Korea Kaskazini Yarusha Kombora Kuelekea Japan

Korea Kaskazini imerusha kombora la masafa mafupi, ambalo ni la tatu kurushwa na taifa hilo katika kipindi cha wiki tatu.

Kombora hilo aina ya Scud lilipaa umbali wa kilomita 450 (maili 280) kabla ya kuanguka katika maeneo ya bahari ya Japan, hatua iliyoifanya Japan kulalamika vikali.

Wachambuzi wanasema jaribio hilo ni ishara kwamba Korea Kaskazini inapiga hatua katika kuunda makombora yanayoweza kubeba mabomu.

Korea Kaskazini imeendelea kukiuka azimio la Umoja wa Mataifa linaloizuia kufanya majaribio yoyote ya makombora au silaha za nyuklia, na imeongeza kasi na idadi ya majaribio hayo katika miezi ya karibuni.

Kikosi cha Jeshi la Marekani katika Bahari ya Pasifiki kimesema kombora hilo lilirushwa kutoka Wonsan, Korea Kaskazini na lilipaa kwa karibu dakika sita kabla ya kuanguka.

Waziri Mkuu wa Japan Yoshihide Suga amewaambia wanahabari kwamba kombora hilo lilianguka katika eneo la bahari lililo kati ya visiwa vya Sado na Oki nchini Japan, katika eneo la pamoja la kiuchumi la visiwa hivyo viwili.

Msemaji wa Jeshi la Korea Kusini amesema kombora hilo lilipaa juu hadi kilomita 120 angani, na tathmini inaendelea kubaini “idadi hasa ya makombora yaliyorushwa,” ishara kwamba huenda nchi hiyo ilirusha zaidi ya kombora moja.

Jaribio hilo la kombora limetekelezwa siku moja baada ya vyombo vya habari vya serikali nchini Korea Kaskazini kusema nchi hiyo ilifanyia majaribio mfumo mpya wa kudungua ndege za kivita, na kutoa picha za kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong-un alishuhudia majaribio hayo.

Polisi Kigambano Wadaiwa Kumuua Mwanafunzi

Askari  wa Jeshi la Polisi, Kituo cha Kigamboni wanadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi tumboni, mwanafunzi wa Chuo cha cha Uvuvi Mbegani, Bagamoyo Boniventure Kimali (25), wakimtuhumu kuwa ni jambazi.

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea saa 3:30 usiku wa kuamkia juzi huko Kigamboni Vijibweni, nyumbani kwa kaka wa marehemu aitwaye, Naftan Barampami ambaye alikuwa akiishi naye.

Akisimulia jinsi ilivyokuwa, Barampami alisema usiku huo wakiwa bado wapo nje ya nyumba yao huku kila mmoja akiendelea na shughuli zake ndogo ndogo na wengine wakiwa wamejipumzisha, ghafla walishangaa kusikia milio ya risasi zilizopigwa mfululizo.

“Tulishtuka, milio hiyo ilitokea upande wa uwanjani ambapo ni jirani na nyumbani kwetu, tuliogopa kila mtu ilibidi atafute namna ya kujiokoa, tulikimbia, mimi nilikimbilia ndani, Boni alikimbia kuelekea nyuma ya nyumba yetu,” alisema.

Alisema akiwa ndani ya nyumba yake alisikia mtu akilia huku akiwasihi watu waliokuwa wamemzingira wasimuue.

“Ikabidi nisogee jirani zaidi na dirisha, nikakaa kwa utulivu na kuangalia nje kupitia dirishani kilichokuwa kikiendelea, ghafla nilimsikia Boni akilia kwa uchungu huku akiugulia maumivu, kumbe walikuwa tayari wamempiga risasi,” alisema.

Alisema askari wote walikuwa wamevaa kiraia, marehemu alikuwa akiendelea kuwasihi wasimuue huku akiwasihi wamuwahishe hospitalini kwani alikuwa akisikia maumivu makali.

“Aliwaomba wampekele hospitali na watujulishe ndugu zake lakini hawakumsikiliza, punde alifika mwenzao ambaye alishtuka na kuwaeleza wenzake wamefanya kosa kwani waliyempiga risasi si jambazi ambaye walikuwa wanamtafuta,” alisema.

Alisema japo alitamani kutoka nje ili akamsaidie ndugu yake lakini alihofia maisha yake kwani mmoja wa askari hao alionya asitokee mtu yeyote katika eneo hilo.

“Niliogopa mno, ikabidi nibaki pale pale dirishani nikifuatilia, nilihofu iwapo nisingetii amri hiyo na kutoka nje na mimi wangenipiga risasi,” alisema.

Barampami  alisema akiwa dirishani hapo, alimshuhudia yule askari aliyefika katika eneo hilo akichukua simu yake na kuwasiliana na wenzake ambao aliwataka wawahishe gari haraka katika eneo hilo.

“Lilipofika, walimchukua marehemu wakampakiza ndani ya gari hilo na kuondoka naye, wakati huo alikuwa bado anaugulia maumivu,” alisema.

Alisema baada ya muda kupita eneo hilo lilikuwa shwari akatoka nje na baadhi ya ndugu zake na kwenda kituo kidogo cha Polisi Vijibweni.

“Pale tuliuliza kama walikuwa wamemfikisha hapo, askari tuliyemkuta alituambia walielekea Kituo Kikuu cha Polisi Kigamboni, tukaenda huko,” alisema.

Alisema walipofika walipokewa na baadhi ya askari waliowakuta ambao waliwaeleza ndugu yao alikuwa amepelekwa Hospitali ya Vijibweni kwa matibabu.

“Tukaenda hadi huko lakini daktari mmoja alituambia hawakumpokea na kumuhudumia kwani hawakuwa na maelezo yaliyojitosheleza, tukarudi Kigamboni lakini awamu hii hatukupewa ushirikiano kama awali, tulipewa amri tusisogee katika eneo hilo,” alisema.

Alisema waliwasiliana na ndugu zao kuwaeleza hali waliyoikuta akiwamo ndugu yao Daudi Gwelenza ambaye anafanya kazi katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

“Tuliwataka wajaribu kupita katika hospitali mbalimbali kumtafuta hasa Muhimbili, ndipo Gwelenza akaenda pale chumba cha kuhifadhia maiti,” alisema.

Gwelenza alisema alipofika hapo alielezwa kuna mwili ambao umefikishwa na askari wa Kigamboni, aliruhusiwa kuuona ndipo akakuta ni ndugu yake huyo.

“Nilimuangalia sura nikakuta ni yeye, nikamwangalia tumboni kweli alikuwa amepigwa risasi eneo la kushoto tumboni, alikuwa na mchanga mwingi wa bahari inaonesha huenda aliburuzwa, nilisikitika mno sikuweza tena kuendelea kuangalia tena,” alisema.

Aliongeza “Lakini nishangaa kwanini katika maelezo yaliyoandikwa juu ya taarifa ya marehemu hawakuandika kwamba amepigwa risasi, waliandika tu amepigwa na waliandika hajulikani jina lake, yaani kama vile walimuokota mahali akiwa ameuwawa.
Katika eneo hilo kulipatikana maganda mawili ya risasi yenye namba 311 (10) na 10 (77).

Msemaji wa familia, Goodluck Kimali ambaye ni kaka wa marehemu, alisema kitendo kilichofanywa na askari hao hakivumiliki.

“Kwa mujibu wa majirani na mashuhuda wa tukio hili, wanasema angewahishwa hospitalini asingepoteza maisha, kwanini hawakumuwahisha huko, kwanini walimpiga risasi tumboni na si mguuni ili asiwakimbie, kwa sababu hakuwa na silaha yoyote, kwanini walimuua,” alihoji.

Alisema tangu kutokea kwa tukio hilo hakuna askari yeyote aliyefika nyumbani hapo kukagua, kujiridhisha juu ya kile walichokuwa wakimtuhumu marehemu.

“Hatujamuona askari hata mmoja kukagua, kwanini hawajafika kufanya ukaguzi, hii inamaanisha wanajua walichokifanya, kitendo hiki hakivumiliki, Tanzania ni nchi ya amani, askari anapaswa kulinda raia na mali zake, lakini imekuwa kinyume chake,” alisema.

Alisema ingawa wanafuatilia kwa ukaribu suala hilo hata hivyo hawaoni kama kweli watasaidiwa kupata haki ya ndugu yao.

“Kuna urasimu mwingi nauona, tunaomba watupe mwili wa ndugu yetu tukampumzishe, maana hata tukisusa na kuwaachia hawawezi kurejesha uhai wake, lakini vitendo hivi vikomeshwe, sisi tunavumilia lakini ipo siku raia watachoka,” alisisitiza.

Alisema watakapokabidhiwa mwili huo, wanatarajia kuusafirisha wakati wowote hadi kijijini kwao Mwayeye, Wilaya ya Buligwe mkoani Kigoma kwa ajili ya maziko.

Mkurugenzi wa Mafunzo na Utafiti wa Chuo cha Mbegani, Ambaksye Simtoe alisema tukio hilo limewashtua kwani marehemu alikuwa kijana mtulivu, msikivu na mpole.

“Alikuwa anasoma kozi ya Uchakataji Samaki, Ubora na Masoko, ngazi ya Diploma, mwaka wa tatu, Juni, mwaka huu angehitimu masomo yake.

“Alikuwa yupo field (mafunzo kwa vitendo) katika Soko la Kimataifa la Samaki Feri, tumesikitika mno, kifo chake kimekuwa cha ghafla hatukutarajia kama ipo siku haya yatatokea,” alisema.

Ijumaa, 26 Mei 2017

Acacia Waipinga Ripoti Iliyowasilishwa Kwa Rais Magufuli kuhusu Madini........ Watoa viwango vyao vya madini kwenye mchanga

Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia imetoa taarifa kwa umma na kueleza kuwa kamati iliyofanya uchunguzi kuhusu mchanga wa madini imepotosha juu ya uwepo wa viwango mbalimbali vya madini kwenye mchanga.

==>Hii ni taarifa yao

By Brad Gordon | Chief Executive Officer | Acacia Mining PLC

Response to this morning’s Press Conference and presentation of the First Presidential Committee’s report on the export of metallic mineral concentrates to the President of Tanzania.

Many of you would have seen this morning’s press conference held at State House at which the First Presidential Committee presented its findings on its investigation into the export of gold/copper concentrates.

The Committee has stated that Acacia has not fully declared all of the minerals contained in the concentrate that it exports and the directive halting the export of metallic mineral concentrates remains in place.

We do not agree with the Committee’s findings which state that the value of minerals within the concentrates in the containers currently at the Dar-es-Salaam port is more than 10 times the amount we declare. We are confident in the accuracy of our declarations which are checked and verified by SGS, which is one of the world’s largest testing companies. The concentrate we produce has some small variances, and each container has different declared quantities of concentrate, but we firmly believe that each container contains on average around 3,000kg of copper, 3 kg of gold and 3 kg of silver. Together, these metals are worth an average of Tsh300 million per container.

We are also a listed company with our accounts being audited extensively by PWC, which verifies that we are fully transparent in everything we do. The revenues we state in our audited accounts match the amount of gold that we declare we produce and sell. If the amount of gold in our concentrates was in line with the Committee findings, then it implies that both Bulyanhulu and Buzwagi would produce more gold than any other mine in the world. Sadly this is not the case.

I appreciate that when events like today happen it creates uncertainty and makes people question who to believe. I want to reassure you that Acacia fully declares everything of commercial value that we produce. We also pay all appropriate royalties and taxes on all of the payable minerals that we produce and that the exporting of the concentrate takes place in full compliance with Tanzanian law and the legal agreements that we have with the Tanzanian Government.

Whilst we have listened to today’s presentation and seen a transcript of the press conference, until we receive a copy of the full report it is difficult to comment on or reconcile the specific numbers and values attributed to Acacia’s metallic mineral concentrates by the Committee, but I repeat, we believe in the numbers we declare.

Whilst we await the report I will respond to one question about royalties that has been raised among the workforce. Under the mining act the Government receives royalties of 4% of the minerals of commercial value namely gold, silver and copper contained in the concentrates. Acacia has always paid the royalty and there is a robust audit trail to demonstrate this. Whilst there are other minerals contained in the concentrate, these are of no commercial value. This is due to the small quantities and the cost to extract them exceeds their value, and so no royalty is due.

Obviously today has been a difficult day for everyone at Acacia. I can assure you that we are doing everything we can to ensure that all of our stakeholders believe in the integrity of Acacia. We have fully declared everything that we produce and have done so since Barrick first entered Tanzania over 15 years ago. We have not cheated the country that we operate in and whose people make up 96% of our workforce. Please continue to work safely as that is the most important thing and I will continue to provide you with updates and hopefully clarity as we move through the coming weeks.

Kafulila Afunguka Baada Ya Profesa Muhongo Kutumbuliwa

Aliyewahi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndugu David Kafulila ameibuka na kutoa ya moyoni baada ya maamuzi yaliyofanywa na Rais Magufuli baada ya kupokea ripoti ya Kamati Maalum kuhusiana na uchunguzi wa makontena 272 ya makinikia yaliyokuwa  tayari kwa kusafirishwa nje ya nchi .
 
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Kafulila ameandika yafuatayo,
  1. Naipongeza Kamati kwa kazi iliyotukuka iliyojaa majaribu ya rushwa kubwa kwani kampuni nyingi madini, mafuta na gas duniani zina sifa hiyo kama alivyopata kusisitiza Profesa Joseph Stirglitz gwiji la uchumi na utandawazi duniani.
  2. Zaidi hatua aliyo chukua Rais kuhusu uharamia huu katika sekta ya madini inapaswa kuungwa mkono na kila mzalendo kwani imekuwa hoja ya upinzani na kila mzalendo kwa miaka mingi iliyoishia kubezwa na kupuuzwa.
  3. Rais asiishie kutaka uchunguzi kufanywa dhidi ya watumishi katika sekta ya madini tu, nchi hii imeoza, uchunguzi ufanywe mpaka ndani ya Idara ya Usalama na vyombo kama TAKUKURU kwani mafisadi hawa waliweka mfumo mzima mfukoni kwa kujenga mahusiano na baadhi ya wanausalama na vyombo vingine vyeti kiuchunguzi.
  4. Namshauri Rais aboreshe Idara ya Usalama kwa kuwa na kitengo cha ujasusi wa kiuchumi (Economic Intelligency) kitakachoweza kumudu kukabiliana na uharamia ktk utoroshaji utajiri wa nchi (illicits flows) kwani nchi inavuja kwa miaka mingi na mtandao wa uharamia huu uliweka sehemu kubwa ya mfumo mfukoni.
  5. Kuna haja yakutazama Katiba yetu upya ili ikibainika hata Rais kama alihusika na ufisadi afikishwe kwenye mkondo wa sheria kwani nchi nyingi za Africa zimeoza kwa ufisadi kuanzia Ofisi Kuu, huko ndio vinatoka VIMEMO kuruhusu uharamia wa namna hii. Ni Ushauri wangu kwa Rais aruhusu mchakato wa Katiba ili pamoja na mambo mengine tuangalie mfumo wa Ofisi Kuu kama moja ya chanzo cha uozo na uharamia huu.
  6. Ni vema Mheshimiwa Rais akatambua kwamba kampuni hizi za kimataifa zinaiba duniani kote ikiwemo Ulaya na Marekani, isipokuwa huku kwetu zinaiba zaidi kutokana na sera duni, sheria dhaifu, mifumo ya usimamizi dhaifu na udhaifu wa wanaopewa nafasi kwa ujumla. Kukabili tatizo hili lazima kutazama kwa mapana na kutengeneza mfumo madhubuti.
  7. Mwisho nimshauri Rais kwamba pamoja na kuchukua hatua hizi za kisheria za ndani, azifikishe kampuni hizi kwenye Mahakama za Kimataifa (Arbitration court) kama inavyo tamkwa kwenye mikataba ili kuzidai fidia kwa miaka yote ya Mikataba yao.
Mitambo na mali zao zishikiliwe mpaka kesi itapomalizika. Na hili lisisomeke kwamba nikukimbiza wawekezaji bali nikukabili uharamia wa utoroshaji rasilimali ambao hata sheria zakimataifa zinapiga vita. Hili ni muhimu sana. Umma una paswa kusimama pamoja dhidi ya uharamia huu!

MIAKA MIA MOJA YA SKAUTI TZ: VIONGOZI WA CHAMA CHA SKAUTI WAKUTANA NA MAKAMO WA PILI WA RAIS WA ZANZIBAR

Chama cha Skauti Tanzania kinatarajia kuadhimisha miaka Mia Moja  ifikapo Tarehe 21 hadi 29 Julai  Mwaka huu  katika Kampasi ya Chuo Kikuu Makao Makuu Mjini Dodoma kwa kushirikisha Vijana wapatao 5,000 kutoka Wilaya zote za Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na zaidi ya wageni 1,000 kutoka Nje ya Tanzania.


SKAUTI MKUU BI. MWAMTUM MAHIZA AKIZUNGUMZA MBELE YA MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR
Mkuu wa Skauti Tanzania Bibi Mwamtumu Mahiza alieleza hayo akiuongoza Ujumbe wa Viongozi  Tisa wa Chama hicho Bara na Zanzibar alipokuwa akitoa Taarifa hiyo kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Vuga Mjini Zanzibar.

Bibi Mwatumu alisema vugu vugu la maadhimisho hayo limekuja kufuatia ziara ya Waziri Mkuu Mstaafu wa Tanzania wa Awamu ya Nne Mh. Mizengo Peter Pinda alipofanya ziara ya kuhudhuria maadhimisho ya Skauti Nchini Uganda Mwaka 2016 na kushawishika na Maadhimisho hayo.

Alisema kutokana na uzito wa maadhimisho hayo Kitaifa yatakayoambatana na maonyesho na mambo mbali mbali Tuzo maalum zitatolewa kwa Marais waliopita pamoja na watu waliofanya ushujaa zaidi katika utekelezaji wa  ujenzi wa Taifa kiuzalendo.

Mkuu huyo wa Skauti Tanzania alimueleza Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar kwamba mipango imeanza kuchukuliwa katika hatua za awali za maadhimisho hayo ambapo Vijana  Kumi wa Skuli za Msingi na Kumi Sekondari wataandaliwa kila Halmashauri za Wilaya Nchini washiriki kwenye tukio hilo muhimu.

Alieleza kwamba Wizara za Elimu, Afya, Mambo ya Ndani, Mambo ya Nje, Tamisemi pamoja na ile inayosimamia Utamaduni kwa upande wa Tanzania Bara zimeshateuliwa  na Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa  kusimamia  jambo hilo la Kihistoria.

Bibi Mwatumu alifahamisha kwamba Mataifa Manne ya Kigeni ambayo ni Korea, Poland, Uganda, na Malawi yameshathibitisha kuhudhuria Maadhimisho hayo.

Akitoa shukrani zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar haina pingamizi kwa Vijana wake katika kushiriki Maadhimisho hayo ya Miaka 100 ya Skauti Tanzania.

Balozi Seif alisema Skauti ni sehemu muhimu na adhimu kwa kuwaandaa Vijana katika muekeo wa kuwa na Utii, Heshima na Maadili mema, lakini kubwa zaidi ni kujengeka katika mazingira ya kuwa Wazalendo kwa Taifa lao.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar aliueleza Ujumbe huo wa Viongozi wa Skauti Tanzania kwamba anaiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar  kutekeleza wajibu wa kulishughulikia suala hilo katika kuwaanda Vijana wa Zanzibar wawe sehemu ya maadhimisho hayo Kitaifa.

Balozi Seif aliupongeza Uongozi huo wa Skauti Tanzania kwa utayari wao wa kuhakikisha lengo la kuanzishwa kwa Chombo hicho muhimu Nchini Tanzania linafanikiwa.

Chama cha Skauti ndani ya Ardhi ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kimeasisiwa Visiwani Zanzibar mnamo Mwaka 1912.



Na. Othman Khamis Ame
  
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar

25/5/2017.

Jumapili, 21 Mei 2017

Tamko la TEF baada ya Star Tv kutangaza kufanya mahojiano na Makonda


Watuhumiwa wa Mauaji Kibiti Watiwa Mbaroni

Mkuu  wa Wilaya ya Rufiji, ambaye pia anakaimu Wilaya ya Kibiti, Juma Njwayo,  amesema vyombo vya dola vimewakamata watu wengi wanaodaiwa kuhusika na uhalifu wa kuua watu katika maeneo mbalimbali ya wilaya hizo.
 
Njwayo amesema licha ya watuhumiwa hao kukamatwa, pia vyombo vya dola vinaendelea kuwasaka watuhumiwa wengine wanaojihusisha na vitendo hivyo.

“Kuna watu wanaoshukiwa ambao ni wengi wamekamatwa na wanaendelea kuhojiwa, kuna wengine wanatafutwa na wakipatikana watahojiwa, lakini hawajakamatwa kwa maana ya kwamba imethibitika wao ni wahalifu,” alisema.

Katika hatua nyingine, aliwataka wananchi wa maeneo hayo waendelee kufanya shughuli zao, lakini kwa tahadhari.

“Watu wanalima, wanaofanya shughuli za Serikali wanafanya, lakini haya yanafanyika tunapata uthibitisho kwa mfano wa hawa watu wanne waliouawa huku Rufiji, kwa hiyo hali iko hivyo. Tunaomba watu sasa wafanye shughuli zao kwa tahadhari, wakiona mtu wasiyemjua watoe taarifa katika vyombo.

“Pia kama wanazo taarifa watuambie, sisi tunajua hawa watu wako kwenye jamii, haiwezekani mtu asiyekujua wewe aje akupige risasi jioni, lazima awe anakujua na kama hakujui basi anashirikiana na mtu anayekujua. Hivyo tunawasisitiza hawa wananchi wetu wawe na tahadhari ya kiusalama,” alisema.

Alipoulizwa amebaini nini katika matukio hayo yanayowalenga zaidi viongozi wa Serikali, alisema suala hilo ni gumu na bado haijajulikana sababu ya uhalifu huo.

“Hatujui sababu ni nini, lakini ni kweli watu wote waliopata hilo tatizo wapo askari, wapo viongozi ama ni wa serikali ya vijiji au chama tawala,” alisema.

Awali, Njwayo alikiri wazi kuwa wananchi katika maeneo hayo wanaishi kwa hofu kwa sababu matukio si ya kawaida.

“Lazima uhofu, yaani upo nyumbani kwako unakula mtu anakuja anakupiga risasi, watu nao wanasikia mlio wa risasi lazima wapate hofu, hilo ni jambo la kila mtu mwenye akili yake timamu lazima ahofie.

“Lakini sisi kwa upande wetu wa wilaya halitupendezi jambo hili, tuna hatua nyingi tunazichukua kwa kushirikiana na Serikali Kuu kupambana na jambo hili,”
alisema.

Kauli ya Njwayo imekuja siku chache baada ya watu wasiofahamika kumuua Mwenyekiti mstaafu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kijiji cha Muyui, Iddy Kirungi, huku mtoto wake, Nurdin Kirungi, akipigwa risasi ya tumbo wilayani Kibiti.

Wauaji hao baada ya kutekeleza unyama huo walitokomea kusikojulikana, hali inayotishia usalama wa raia na mali zao, huku wengine wakilazimika kuzikimbia nyumba zao kwa hofu ya kupoteza maisha.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema linaendelea kuwasaka wahalifu na kuimarisha ulinzi.

Rais Magufuli akabidhi Uenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Rais Museveni wa Uganda

Rais John Magufuli leo (Jumamosi) amemkabidhi rasmi uenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), kwa Rais Yoweri Museveni.
 
Muda mfupi kabla ya kumkabidhi nafasi hiyo, Rais Magufuli ambaye alikuwa mwenyekiti wa EAC kwa miaka miwili amewashukuru wanachama wa jumuiya hiyo kwa kumuamini na kumpa nafasi hiyo miezi michache baada ya kuingia madarakani.
 
“Mliniamini mkanichagua licha ya kuwa madarakani kwa muda mfupi,”amesema Rais Magufuli ambaye aliteuliwa kuwa mwenyekiti wa EAC, mapema mwaka jana.
 
Rais Magufuli amesema anaimani na Rais Museveni kuwa atafanya kazi nzuri kutokana na uzoefu wake.
“Yaliyonishinda kuyatatua, atayatatua yeye (Rais Museveni),”amesema.
 
Mara baada ya kukabidhiwa nafasi hiyo, Rais Museveni ambaye sasa ni mwenyekiti wa EAC amesema atahakikisha anatumikia nafasi hiyo kwa nguvu na uwezo wake wote.

Watanzania 11 Watiwa Mbaroni Afrika Kusini Wakituhumiwa Kumbaka Mwanamke Mjamzito

Wanaume 11 ambao ni raia wa Tanzania wamekamatwa na Polisi na kufikishwa Mahakamani wiki hii Johannesburg Afrika Kusini .

Radio na Mtandaoni Johannesburg wiki hii kumeripotiwa kuwa kosa lililofanya Wanaume hao 11 kukamatwa na Polisi ni kumbaka Mwanamke mjamzito mwenye umri wa miaka 22 aliyekua akitoka kazini saa kumi na moja alfajiri.

Mwanamke huyo alikua akitoka kazini na Mfanyakazi mwenzake ambaye ni Mwanaume ambapo ghafla walivamiwa na kundi la Wanaume wenye silaha za moto na wakamvuta Mwanamke huyo kabla ya kumpiga Mfanyakazi mwenzake ambae baadae alifanikiwa kutoroka.

Baada ya Mfanyakazi huyo kutoroka aliwapigia simu Polisi na wakafanikiwa kuwahi eneo la tukio na kukuta Wanaume hao wakimbaka kwa zamu Mwanamke huyo mwenye ujauzito wa miezi mitatu.

Polisi wapatao kumi waliingia kwenye jengo tukio lilikofanyika na kumuokoa Mwanamke huyo aliyekua kwenye hali mbaya ambapo walimpeka Hospitali huku Watuhumiwa wakichukuliwa na kupandishwa Mahakamani siku ya Jumatano.

Ijumaa, 19 Mei 2017

Serikali Yatolea Ufafanuzi Kazi Ya Ofisi Ya Mdhibiti Na Mkaguzi Wa Hesabu Za Serikali

Na Benny Mwaipaja, WFM-Dodoma
Serikali imeeleza kuwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haijawahi kumuhusisha Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ukaguzi wa Balozi au ukaguzi wowote ule kama Umoja wa Mataifa kwa sababu hakuna ulazima wa kufanya hivyo Kikatiba na Kisheria.

Hayo yameelezwa Bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango (MB), Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kiwengwa Khamisi Mtwana Ally (CCM), aliyetaka kujua ni mara ngapi Ofisi hiyo ya Bara imeishirikisha Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Zanzibar.

Akijibu swali hilo Dkt. Kijaji alisema kuwa, Ofisi hizo kila moja ina mipaka yake ya kufanya ukaguzi na kwamba jukumu la ukaguzi wa Taasisi za Muungano lipo kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

“Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali imeanzishwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na kwamba majukumu ya Ofisi hiyo yameainishwa katika ibara ya 143(2) ya katiba hiyo”. Alisema Dkt. Kijaji

Dkt Kijaji aliongeza kuwa, eneo hilo linamtaka Mdhibiti na Makguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kufanya ukaguzi angalau mara moja kila mwaka na kutoa taarifa kuhusu ukaguzi wa Hesabu za Serikali, Bunge na Mahakama.

Aidha, Dkt. Kijaji alisema kuwa majukumu hayo yameainishwa katika kifungu cha 10 cha Sheria ya Ukaguzi wa Umma ya mwaka 2008 na kanuni zake za mwaka 2009.

Dkt. Kijaji alifafanua kuwa, ukaguzi wa Balozi unafanyika chini ya fungu 34, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kuwa Ofisi zote za Ubalozi ni sehemu ya fungu 34.

“Hivyo basi, ukaguzi wa Balozi kama ilivyo kwa Taasisi nyingine za Muungano unafanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .”alisema Dkt. Kijaji

Aliongeza kuwa, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Zanzibar, majukumu yake yameainishwa kwenye ibara ya 112 ya Katiba (3) ya katiba ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Akiongeza majibu ya swali hilo, Waziri wa Mazingira na Muungano, Januari Makamba alisema kuwa wakaguzi wa pande zote kutoka Tanzania Bara na Visiwani hufanya kazi kwa kushirikiana katika mambo ya ukaguzi wa hesabu za serikali.

Katika swali la nyongeza Mbunge wa Mkwajuni, Ally Zubeir Ngwali (CUF), alihoji ni kwanini fedha za mfuko wa Jimbo hazijawahi kukaguliwa na zitakaguliwa kwa utaratibu upi.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jaffo alisema upo utaratibu maalum wa kushughulikia mambo hayo.