Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumanne, 9 Mei 2017

Mbunge Catherine Ruge Aanza Kwa Kuihoji Serikali Juu ya Usawa kwenye Uwekezaji mkoani Mara

Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mhe Catherine Ruge ameanza kutumikia uteuzi wake Bungeni kwa kuihoji serikali kuhusu mkakati wake wa kuwekeza kwa usawa mkoani Mara.
Katika swali lake la nyongeza lililoelekezwa kwa Wizara ya Maliasili na Utalii, Mhe Ruge aliuliza,  “Mkoa wa Mara una vivutio vingi hasa kwa Eastern Corridor (ambao ni Upande ulio na Hifadhi ya Serengeti) na Western Corridor (Upande ulio na Ziwa Victoria), lakini serikali imewekeza zaidi kwa Eastern Corridor Upande wa Hifadhi kuliko Western Corridor Upande wa Ziwa Victoria ambao ni kama umeshaulika, Je ni nini mkakati wa serikali kuhusu Upande wa Ziwa Victoria na kwa kuzingatia vivutio vingi vya asili vinapatikana ndani yake? Na Je serikali INA mpango gani kuendeleza Upande wa Ziwa Victoria?”
Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Mhe Catherine Ruge akila kapo na kuwa Mbunge kamili mbele ya Spika wa Bunge, Job Ndugai. Mhe Ruge ameteuliwa kuwa Mbunge Maalum kujaza nafasi iliyokuwa wazi kufuatia kifo cha Mbunge Elly Macha aliyefariki 31.03.2017.
Mbunge huyo pia kupitia ukurasa wake wa Facebook wa Catherine Ruge alitoa wito kwa Watanzania wenye uzoefu na mazingira ya ziwani na vyanzo kutoa mapendekezo na maoni yao ili kwa pamoja waweze tambua namna ya kuwasilisha kwa Waziri wa Wizara husika.
“Niombe maoni yenu kwa watu mlio na uzoefu na mazingira ya Ziwani na vyanzo vyake vya mapato ili kwa pamoja tushauriane niwe na cha kusema baadae. Kwasababu Waziri wa Wizara husika ameniomba nionane nae kwa maoni na mawazo niliyonayo kwa vyanzo vinavyopatikana Ziwani.
Ahsanteni sana. Karibuni” aliandika Mhe Ruge.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni