Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumatatu, 27 Februari 2017

Skauti yazindua Mradi wa “U-Report” kwa ushirikiano na UNICEF

Chama cha Skauti Tanzania, kimezindua programu mpya iitwayo “U-Report”, mradi huu ni miongoni mwa miradi inayofadhiliwa na UNICEF ambapo upo katika nchi nyingi za Bara la Afrika ata Ulaya.

Viongozi wakionyesha bango lenye namba ambayo inatumika kwa kujiunga na “U-Report” katika uzinduzi wa mradi huo uliofanyika tarehe 25/02/2017, wa pili kutoka kulia ni Abdulkarim Shah (Kamishna Mkuu wa Skauti) akifuatiwa na Omary Mkali (mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia) wa pili kutoka kushoto ni Rashid Kassim Mchatta (Naibu Kamishna Mkuu, aliyevaa fulana nyeupe), Emmanuel Bayo (mwakilishi kutoka UNICEF, aliyevaa fulana nyeusi) Wa kwanza kulia ni Joackim Assenga (Kamishna wa Skauti Wilaya ya Temeke) na wa kwanza kushoto ni Omary Mavula (Msaidizi wa Kamishna Mkuu wa Skauti Programu ya Vijana)

Chama cha Skauti Tanzania, kimezindua programu mpya iitwayo “U-Report”, mradi huu ni miongoni mwa miradi inayofadhiliwa na UNICEF ambapo upo katika nchi nyingi za Bara la Afrika ata Ulaya, mradi wa “U-Report” umezinduliwa wakati wa maadhimisho ya wiki ya kumbukumbu ya mwanzilishi wa skauti duniani “Founders day” katika viwanja vya Makao Makuu ya Skauti Tanzania, Upanga, Dar es Salaam, tarehe 25 Februari 2017.

U-Report ni programu maalum kwaajili ya kuripoti matukio mbali mbali yanayotokea kwenye jamii zetu kama vile unyanyasaji wa watoto/kijinsia, matukio ya uhalifu, ajira za utotoni, ukatili dhidi ya watoto.
Aidha, imetolewa rai ya kujiunga kwa kutuma sms yenye neno “Sajili” kwenda namba “15070” sms zote ni Bure (bila ya kutozwa gharama yoyote), huduma hii inapatikana kwa watumiaji wa mitandao ya simu ya kiganjani ya Tigo, Vodacom, Airtel, Zantel aidha mradi huo unatarajia kujiunga na mitandao mingine ya simu ya kiganjani ya Halotel pamoja na TTCL.

Katika uzinduzi huo ulioambatana na kuazimisha wiki ya kumkumbuka mwanzilishi wa Skauti duniani Robert Baden-Powell (a.k.a BP) aliyezaliwa tarehe 22 Februari 1857. Ambapo kwa Tanzania Bara uliingia mwaka 1917, takribani Skauti zaidi ya 5000 waliudhuria kutoka Mkoa wa Dar es Salaam na baadhi kutoka mkoa wa Pwani.

Habari na Murtadhwa El bahsan
Picha na PR Lab (TSA)



















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni