Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumapili, 11 Februari 2018

WATENDAJI WA ARDHI WAZIMIA BAADA YA KUSHINDWA KUTOA MAJIBU KWA RC MAKONDA

Watendaji wa Ardhi wa Manispaa za Jiji la Dar es salaam leo *wamejikuta kwenye wakati mgumu* baada ya kupata *kigugumizi na kushindwa kujibu maswali ya msingi* yaliyokuwa yakiulizwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe. Paul Makonda* kuhusu idadi ya *Migogoro ya Ardhi* katika idara wanazoongoza na kusababisha baadhi yao *kudondoka kwa kuzimia na kukimbizwa hospital.*

Kitendo cha *wakuu hao wa idara* kushindwa kujibu *maswali* ambayo yamekuwa chanzo cha *migogoro ya ardhi* isiyoisha *kimewakera Maelfu ya wananchi* waliojitokeza kwenye ukumbi wa *Diamond Jubilee* kwaajili ya kujua *hatma ya Malalamiko* yao na kujikuta wakuomba *RC Makonda* kuwatumbua.

Kutokana na watendaji hao kushindwa kutekeleza majukumu yao *RC Makonda* ameagiza *wakuu wa idara ya ardhi Manispaa za Ubungo na Ilala* wapangiwe kazi nyingine kutokana na *kushindwa kutekeleza majukumu yao.*

Aidha *RC Makonda* amesimamisha shughuli zote za *Mabaraza ya Kata Dar es salaam* kuwakuwa hazina *uwezo wa kusikiliza kesi* na pia hawana *wataalamu wa sheria* kitendo kinachochangia *Migogoro mingi ya Ardhi*.

Kutokana na hilo *RC Makonda* amewataka *Makatibu Tarafa* kuanza kutembelea Mabaraza hayo kuanzia Jumatatu ya *February 12.*

*RC Makonda* amechukuwa uamuzi huo wakati wa kupokea *Ripoti ya Malalamiko ya Wananchi* waliodhulumiwa Haki zao ambapo zaidi ya *Wananchi 11,652* walifika kwaajili ya kupata *Msaada wa kisheria* ambapo jumla ya *malalamiko 3,373* yalipokelewa na kusikilizwa huku *wananchi waliosikilizwa wakiwa ni 6,052* na ambao hawakupata fursa ya kusikilizwa wakiwa ni *Wananchi 5600* ambapo leo *RC Makonda* ameandaa utaratibu wa kuhakikisha *wote wanasikilizwa.*

*RC Makonda* amesema *idadi kubwa ya wananchi* waliokimbilia kwake kutafuta haki ni tafsiri tosha kuwa *baadhi ya watendaji hawasimami ipasavyo* katika nafasi zao ambapo amewaagiza *Wakurugenzi kuanza kupitia wasifu wa wakuu wa idara CV na kazi zote wanazofanya.*

Ili kuhakikisha wanyonge walioporwa haki zao wanazipata *pasipo kuvunja sheria RC Makonda* amewasilisha kwa Kamanda wa Polisi kanda maalumu ya Dar es salaam *Majina ya watu wenye michezo ya kudhulumu wananchi* kwaajili ya kuchukuliwa *hatua za kisheria.*

*Makonda* ameagiza Watendaji kuhakikisha malalamiko yote ya wananchi ya *Migogoro ya ardhi, Mirathi,Talaka, Madai, Makosa ya jinai, Masuala ya kazi, Ubakaji na utapeli* yanafanyiwa kazi kabla ya mwezi April.

Aidha amewataka *madalali wote wanaofanya kazi ya kutekeleza hukumu za Mahakama au Bank* kufika ofisini kwake siku ya jumanne wakiwa na *nyaraka za usajili.*

Nao baadhi ya Wananchi waliofika kwenye mkutano huo *wamefurahia* hatua za *RC Makonda* katika kuwajali *wananchi wanyonge* ambapo pia wameshukuru *mkutano huo umewasaidia kujua kwa undani masuala ya kisheria*.

Aidha wamesema kuwa wanaamini kwa ujasiri *RC Makonda* wanafarijika kuona *tabu waliyoipata kwa miaka mingi wakitafuta haki yao inaenda kupatikana*.

*HUU NDIO UONGOZI THABITI UNAOACHA ALAMA, PONGEZI KWAKO RC MAKONDA*

Jumapili, 4 Februari 2018

Wafanyakazi waanza kukatwa mishahara kufadhili uchaguzi wa 2020


Wafanyakazi wa umma nchini Burundi wameanza kukatwa asilimia 10 ya mishahara yao kwaajili ya kufadhili uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwaka 2020.

Katika kipindi cha miaka miwili ijayo, raia wote wa Burundi walio na zaidi ya umri wa kupiga kura wa miaka kumi na minane na zaidi, ni sharti wachangie katika hazina hiyo ya kitaifa.

Serikali ya Burundi imesema imechukua uamuzi huo ili kuziba pengo lililosababishwa na uamuzi wa wafadhili wa kuzuia misaada tangu mzozo wa mwaka 2015 wakati rais Pierre Nkurunziza alipowania muhula wa tatu.

Hata hivyo serikali imekariri kuwa hazina hiyo ya uchaguzi ni wazo la raia wa Burundi wenyewe, pendekezo ambalo limepingwa na wakuu wa vyama vya wafanyakazi.

NDALICHAKO: MLITUELEWA VIBAYA, MICHANGO SHULENI INARUHUSIWA