Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Ijumaa, 24 Agosti 2018

Wananchi Waishi Nje Baada Ya Nyumba Zao Kchomwa Na Kubomolewa

Na John Walter-Manyara
Wakazi wa kijiji cha Manyara kata ya Magara  eneo la kambi ya fisi wilayani Babati mkoani Manyara wamejikuta wakilala katika mahema baada ya makazi yao kuchomwa moto na Kubomolewa na serikali kwa maelezo kuwa maeneo wanayoishi  ni ya hifadhi ya ziwa Manyara.

Kituo hiki kilifika katika kijiji hicho ambacho kipo pembezoni mwa ziwa Manyara na kukuta majivu ambapo nyumba 86 zimeteketezwa kwa moto na kubomolewa.

Wakizungumza na kituo hiki wanakijiji hao walieleza kuwa hawajui kwanini wamebolewa nyumba zao ili hali wameanza kuishi tangu miaka ya 1984,zaidi ya miaka 30 sasa.

Baadhi yao wamesema hawakuwepo wakati zoezi hilo la kuchoma na kubomoa nyumba likiendelea wamekuta vitu vyao vikiwa nje huku badhi vikiwa vimeteketea kabisa.

Akielezea Mgogoro huo kati ya kijiji na Halmashauri ya wilaya  Mwenyekiti wa kitongoji hicho Wiliam Muna amesema kuwa mgogoro huo umeanza tangu mwaka 2013.

‘’Alama za mpaka wa kijiji ziliwekwa mwaka 2003 baada ya hapo pakawa na marekebisho ambapo wananchi walipewa maeneo haya na kukabidhiwa risiti na Halmashauri ya kijiji’ alisema Muna.

Muna alisema ‘’Mimi kama kiongozi wa kitongoji jambo hii imeniumiza sana kwani wananchi wamekosa haki zao,na hata fidia hawakupatiwa.’’

Aliendelea kusema kuwa Maeneo hayo yamechukuliwa na mwekezaji kutoka  Jumuiya ya uhifadhi wanyamapori [Juibu].

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Babati Hamisi Iddy Malinga alifika katika eneo hilo na kueleza kuwa wameamua kuwaondoa kwa nguvu wananchi hao kwa kuwa wamefanya hivyo kuwaondoa ili kuendelea kulilinda ziwa Manyara.

Suala ambalo limejitokeza kwenye ekolojia wa Tarangire Manyara ni uharibifu wa Ziwa Manyara lakini pia  ushoroba unaounganisha Tarangire-Manyara.

Malinga amesema Katika eneo la kijiji cha  Manyara kumekuwa na vijiji kadhaa ambavyo siku ya nyuma  waliingia mpaka kwenye maeneo ya uhifadhi [eneo la kijani] lakini baada ya serikali kuwatangazaia waliondoka lakini imekuwa vigumu kijiji cha Mnayara kutii agizo hilo.

Mpaka sasa wanakijiji hao wamejikusanya kwa majirani wakiwa na watoto wao huku kukiwa na hofu ya kupata magonjwa ya milipuko kama vile kipindu pindu na kuhara kwani hakuna vyoo hali inayowalazimu kujisaidia vichakani.

Jumatano, 1 Agosti 2018

RSA TANZANIA YAKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI

Mhe. Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi akikabidhiwa T-Shirt ya mabalozi wa Usalama Barabarni na viongozi wa RSA Tanzania

Leo tarehe 1 Agosti 2018, Uongozi wa RSA Tanzania ukiongozwa na Mwenyekiti wake John Seka na Wakurugenzi Abdulkarim Shah, Ally Nurdin, Marlin Komba, Augustus Fungo pamoja na Isabela Nchimbi mjumbe kutoka TAWLA, akiwakilisha Asasi nyingine zinazojishughulisha na mpango wa marekebisho ya sheria ya Usalama Barabarani, umeonana na Mhe. Kangi Lugola Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ofisini kwake Jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo hayo, viongozi wa RSA waliitambulisha RSA Tanzania na Muungano wa Asasi za kiraia zinazoshughulikia usalama barabarani. Pia walimpongeza Mhe. Lugoka kwa kuteuliwa kushika wadhifa huo na hatua mbalimbali anazochukua kuhakikisha usalama barabarani unaimarika.

Aidha, viongozi walimweleza mheshimiwa Waziri changamoto mbalimbali zinazokabili usalama barabarani, na zile zinazokwamisha ufanisi wa taasisi na kutoa mapendekezo ya namna zinavyotakiwa kukabiliwa kiutendaji na kupitia mabadiliko ya sheria ya usalama barabarani.
Viongozi walimkaribisha mhe. Waziri katika RSA na katika Maadhimisho ya Siku ya Mabalozi wa Usalama Barabarani yatakayoadhimishwa 11.08.2018 jijini Dodoma.

Kwa kumkaribisha RSA Tanzania viongozi walimkabidhi Mhe. Waziri, sare ya RSA Tanzania.
Mhe. Waziri aliwashukuru mabalozi kwa kazi nzuri wanayoifanya, akawakaribisha kufabya kazi naye na kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kukabiliana na ajali. Akaongeza kuwa atatoa ushirikiano wa kutosha kwa taasisi kwa kuhakikisha pamoja barabarani kunakuwa salama.

Baada ya hapo viongozi walipiga picha ya pamoja na kuagana na mhe. Waziri.
RSA Tanzania
Usalama Barabarani ni Jukumu Letu Sote

Picha na Ally Nusrdin (Ally Six)