Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Alhamisi, 4 Mei 2017

Chadema wamteua Catherine Ruge kuwa Mbunge

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imemteua Catherine Nyakao Ruge kuwa mbunge viti maalumu kupitia tiketi ya Chadema.

Taarifa iliyotolewa ya Nec imesema kuwa imemteua Ruge baada ya kukamilisha kikao ilichokifanya leo.

Katika taarifa hiyo Nec imeeleza kuwa kikao hicho kilifanywa kwa mujibu wa Ibara ya 78(4) ya Katiba ya Tanzania 1977 pamoja na Kifungu cha 86A (8) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343.

Uteuzi wa Ruge umefanyika baada aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Dk Elly Macha kufariki dunia Machi 31, mwaka huu.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni