Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumatatu, 8 Januari 2018

BIG NEWS: VIBOKO 12 KWA ATAKAE SIMAMA NA MWANAFUNZI, NA FAINI .........

TAHADHARI
BAKORA ZITAKUHUSU


Kama wewe ni kijana wa kiume usisimame na wanafunzi wa like, ukionekana tu utachapwa viboko 12 au faini Tshs. 10,000

Ukiwa katika kata ya Ihungwe wilayani Sengerema usithubutu kusimama na mwanafunzi wa kike, ukikamatwa utachapwa viboko 12 au faini ya 10,000 baada ya viongozi wa kata hio kupitisha rasmi sheria hio  katika kikao chao cha baraza la maendeleo ya kata kilichofanyika hivi karibuni, kufuatia tatizo la kupata mimba wanafunzi wa kike kuzidi kuwa sugu.

Sheria hio  ndogo imepitishwa ikitanguliwa na agizo la Mkuu wa wilaya ya Sengerema Nd. Emanuel Kipole alieagiza Wanaume watakaokutwa na wanafunzi wa kike  wapigwe bakora 12 au faini ya Tsh.10,000, agizo hilo  alilitoa mwezi oktoba mwaka 2017

Chanzo: Gazeti la Mwananchi.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni