Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Jumatano, 3 Januari 2018

MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA 2018



Baraza kuu la Taifa la Chama cha Skauti Tanzania litakuwa na Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Viongozi utakaofanyika tarehe 22.02.2018 Dar Es Salaam katika ukumbi wa Karimjee Hall.

Wajumbe halali watakaohudhuria Mkutano huu ni kwa mujibu wa Katiba ya Chama 2017 Ibara 5.2.1 na 5.2.2. Wajumbe wote watatakiwa kuripoti Makao Makuu ya chama tarehe 22.02.2018 saa 01:00 asubuhi. Wajumbe husika toka Mikoani ni sita
(watatokana na Mkutano Mkuu au kwa ushauri kati ya Bodi na Kamati Tendaji ya Mkoa).

Mkutano utakuwa na Ajenda zifuatazo:
a. Kuthibitisha mihtasari ya mikutano ifuatayo:
i. Mkutano Mkuu wa Baraza wa tarehe 25.08.2015
ii. Mkutano Maalum wa Baraza wa tarehe 28.07.2017
b. Yatokanayo na mikutano fuatayo:
i. Mkutano Mkuu wa Baraza wa tarehe 25.08.2015
ii. Mkutano Maalum wa Baraza wa tarehe 28.07.2017
c. Taarifa ya Kamishna Mkuu ya mwaka 2016 hadi 2017
d. Taarifa ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2016 na 2017
e. Mapendekezo ya Mabadiliko ya P.O.R ya Chama cha Skauti Tanzania.
f. Uchaguzi wa viongozi wa Chama

Sifa na fomu za kugombea nafasi tajwa zinatolewa na kurejeshwa Makao Makuu ya chama kuanzia tarehe 02 Januari, 2018 hadi 15 Januari, 2018 . Pia zinapatikana kupitia www.tanzaniascouts.org / www.scout.org/tanzania / www.DaresSalaamlocalscout.blogspot.com na elbahsan.blogspot.com Mwisho wa kurejesha fomu
Makao Makuu ni tarehe 15 Januari, 2018 saa 10:00 Jioni.

Wajumbe watajigharamia usafiri na malazi . Chama kitarejesha Tshs 100,000/= kwa
kila mjumbe kama posho ya kujikimu.

Wako katika Skauti
Eline Kitaly
KAMISHNA MTENDAJI

soma Hapa kwa habari zaid

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni