Powered by: Elbahsan Web & Blog Designer
Do want your Network!!! Website or Blog-Spot, Try Us: Elbahsan Web & Blog Designer Contact Us Now... Calll; +255743550360 | +255788680558 Email; murtadhaalbahsan@gmail.com

Zawamba Photo Production

Ijumaa, 5 Januari 2018

MTOTO WA MZEE KINGUNGE AKANUSHA TAARIFA ZA KIFO CHA BABA YAKE ZINAZOSAMBAA MITANDAONI..

Mtoto wa mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombae Mwiru,Tonny Ngombale Mwiru amekana taarifa zinazozagaa mitandaoni kuhusu kifo cha baba yake mzee Kingunge Ngombale Mwiru.

Tonny amefanya mahojiano na waandishi wa habari jioni ya leo na kuwaeleza kuwa baba yake yuko hospitali akipata matibabu baada ya kung’atwa na mbwa hivyo kupata majeraha Kwenye miguu ambayo ndiyo anayouguza hospitalini kwa sasa.

Kuhusu mazishi ya mke wa mwanasiasa huyo ambaye alifariki jana katika hospitali ya Muhimbili Tonny Ngombale Mwiru amesema familia itatoa taarifa mapema kesho baada ya baba yao mzee kingunge kuelezwa na kutoa maelekezo kama baba mzazi na kiongozi wa familia hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni